Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke-1

WANAUME wengi wanaamini wanawake, kwa kawaida, ‘wanapenda hela.’ Kwamba ukiweza kumhakikishia mwanamke 'uhakika wa kiuchumi' unakuwa umemaliza. Ingawa hatuwezi kupuuza ukweli kuwa uhakika wa 'kiuchumi' ni moja wapo ya mahitaji ya mwanamke, lakini si sahihi kuamini kuwa moyo wa mwanamke unaweza kuthamanishwa kwa fedha.
Fikra hizi walizonazo wanaume [kuwa anachokihitaji mwanamke ni fedha] zimeleta matatizo mengi katika mahusiano na ndoa. Kwa mfano, wapo wanaume ambao baada ya kuhakikisha wenzi wao wamepata mahitaji ya msingi, basi wanawatelekeza kihisia. Hali hii husababisha upweke mkubwa kwa wanawake hawa wanaojikuta hawana mtu wa karibu kuwasikiliza isipokuwa vitu.

PICHA: hotnaijanews
Upweke, kwa hakika, huzaa migogoro isiyokwisha inayowafanya wanaume [ambao kimsingi ndio wasababishi wa upweke huo] washindwe kuwaelewa wanawake. Kwa mtazamo wao, ni vigumu kumridhisha mwanamke. Wengine wanaenda mbali na kufikiri , 'mwanamke ni kiumbe mgumu kueleweka' kwa sababu, ‘hata ufanye nini...hata umpe nini hawezi kuridhika’.
Lakini wanachosahau wanaume wenye mawazo haya ni kuwa mwanamke kwa asili yake anayo mahitaji ya msingi ambayo yanapopuuzwa, chochote kinachofanyika kama mbadala wa mahitaji hayo hakiwezi kuwa na maana yoyote. Usipoweza kujua mahitaji yake halisi, unaweza kumpa chochote kile unachodhani anakihitaji na bado mambo yasiende kama unavyotamani iwe. 

Kusema hivyo, haimaanishi sielewi kuwa wapo wanawake wengi wanaopenda kujipatia fedha kwa wanaume. Hawa ni wanawake wanaofanya biashara ya mahusiano.  Kwao, hakuna sababu yoyote ya kuwa na uhusiano imara na wenzi wao isipokuwa mpangilio wa kujipatia vitu na fedha. 
Hatuzungumzii uhusiano huo wa kibiashara kati ya mwanamume na mwanamke bali uhusiano wa dhati unaojengwa katika misingi ya upendo, uaminifu, kuelewana na ahadi ya kuwa pamoja katika dhiki na raha.
Hebu na tutazame mahitaji makubwa ya kihisia aliyonayo mwanamke mwenye upendo wa dhati kwa mwenzi wake.

Kupendwa kwa vitendo

Tulishaona kuwa hadhi ya mwanaume inategemea kwa kiasi kikubwa namna anavyoheshimiwa. Kwa mwanamke hali ni tofauti. Hadhi yake inategemea namna anavyopendwa na mwenzi wake. 


Upendo kwa mwanamke unaeleweka anapoambiwa bila kuchoka na kuthibitishiwa kwa kutendewa vitendo kuwa anapendwa. Katika lugha ya kiingereza, hapa tungetumia neno affection, yaani matendo yanayoonesha mapenzi kwake.
Hata hivyo, lugha ya mapenzi hutegemea mambo mengi. Kuna athari za utamaduni, desturi na imani zilizopo katika jamii aliyokulia mwanamke. Hata hivyo, yapo matendo yaliyothibitika kuvuka mipaka ya kiutamaduni. 
Mfano, kumwambia mwanamke unampenda mara nyingi iwezekanavyo, ni hitaji la msingi. Kwa mwanamume, kuambiwa anapendwa inaweza isiwe jambo la maana, lakini si kwa mwanamke. Mwanamke anatamani kusikia mara nyingi kadri inavyowezekana kuwa anapendwa. 

Pia kuna vitu kama kupewa zawadi asizotarajia, kutumia muda wa mapumziko pamoja nae, kutoka naye kwenda mbali na nyumbani na mambo kama hayo yanayoonesha kuwa kweli unampenda.
Ndio kusema, ikiwa unataka kuugusa moyo wa mwanamke, akupe heshima unayoihitaji kama mwanaume, unawajibika kujua vitu gani mahususi ukimfanyia vinatuma ujumbe wa wazi kuwa unampenda. Usipoweza kumfanya mwanamke ajisikie kupendwa, anapoteza hamu ya uhusiano. Huchoka kihisia na anaweza kufanya mambo yasiyotarajiwa ili tu kuhujumu mahusiano. 
Anataka kuwa kipaumbele chako

Mwanamke hapendi kujikuta katika mazingira ya kushindania nafasi ya kwanza na kitu kingine chochote iwe ni kazi, mtu au chochote kile unachokipenda wewe mwanamume. 


Tulishaona kuwa kwa mwanaume, hadhi yake hutegemea zaidi namna uwezo wake unavyotambuliwa. Hali hiyo humfanya mwanamume atumie muda mwingi kufanya mambo yanaweza kumpa heshima katika jamii. Inaweza kuwa kazi, biashara, mamlaka na namna zozote zile zinazomwongezea uwezo. 

Lakini wakati anapotumia muda mwingi katika mambo hayo, ni rahisi kuonekana ameyafanya mambo mengine kuwa ya muhimu kuliko uhusiano wake na mwenzi wake. Wanawake wengi hawapendi kujikuta katika hali hii. Hapa ndiko iliko tofauti. 

Mwanamke hatamani kuwa kwenye nafasi ya ‘mengineyo’, ‘ziada’, ‘baadae’ ‘nikipata muda’. Unapomweka 'akiba' mwanamke hawezi kufurahia kwa sababu anatamani awe kipaumbele chako.

Mambo mengi huthibitisha kuwa umempa nafasi ya kwanza. Mfano kuwa na muda wa kuwa naye mara nyingi kadri inavyowezekana, kuahirisha mambo mengine ya muhimu kwa ajili yake, kuwahi miadi unapoahidi kukutana nae, kuwasiliana naye kwa karibu na mambo kama hayo. Unaposhindwa kufanya hivyo, mwanamke hupata ujumbe kuwa yeye ni mtu wa ziada baada ya mambo ya muhimu.
Kadhalika, ili kumwambia yeye ni kipaumbele, mwanamke anatamani kila unapoongea nae akili yako yote iko pamoja naye. Kuwa pamoja naye maana yake ni kuachana na vyote vinavyokuondolea uzingativu na kumsikiliza kwa makini.

Mwanamke anatamani unapozungumza naye ufuatilie anachokisema, umpe mrejesho kuwa unamwelewa na uonesha kuwa mwili, akili, hisia ziko pamoja naye kumsikiliza. Vinginevyo, mwanamke anakuoana kama hujaweza kumpa nafasi yake anayoistahili.
Inaendelea


Fuatilia gazeti la Mtanzania, safu ya Saikolojia kila Alhamisi, kwa makala kama hizi.

Maoni

  1. PROAKUN.WIN | AGEN BANDARQ | QQ ONLINE | DOMINOQQ | BANDARQ ONLINE | JUDI ONLINE TERBAIK DI INDONESIA, adalah Website Rekomendasi Situs Situs Terbaik dan Ternama dengan Hasil Winrate Teringgi Terbaik Di Indonesia.

    Agen BandarQ
    QQ Online
    DominoQQ
    BandarQ Online
    Judi Online

    JibuFuta
  2. Mawazo mazuri sana na yanajenga. Kwa vijana ambao tuko kwenye mipango mikakati ya kuelekea huko hatuna budi kuyashika yote hayo na kuyafanyia kazi.

    JibuFuta
  3. Mpenzi wangu aliachana na mimi, najua ilikuwa kosa langu ambalo lilimfanya aachane na mimi, akanipata nikiongea juu yake, kuna kijana niliyemwita rafiki yangu alinivuta na kufanya naye mapenzi kisha mpenzi wangu akatushika, basi aliachana na mimi, ninampenda sana, nilifurahisha kwa wiki na miezi hakukubali kunikubali, nilikuwa nikisoma mkondoni jinsi ya kumrudisha mpenzi wangu basi nilikuta na makala juu ya jinsi mwanamke alirudi Mumewe aliyempa talaka, alisema kuwa Dk Lomi amsaidia alifanya sala kadhaa na mumewe amerejea kwake, basi na mimi nikawasiliana na Dr Lomi na kuelezea kile kilichotokea kisha akanisaidia kufanya maombi kadhaa na mpenzi wangu akarudi akiniombea alijuta kuwa bado ananipenda na leo tumerudi pamoja na naahidi kamwe hatutazungumza juu yake na leo tunafurahi, ikiwa unahitaji pia Msaidizi wa Dk Lomi kuwasiliana naye kwenye Line ya nambari ya WhatsApp; 2349034287285 unaweza pia kumtumia barua pepe; lomiultimatetemple@gmail.com kwa msaada

    JibuFuta
  4. Hayo yaloandikwa kwenye makala ni mazuri,ila kuna watu tulishafanyaga yote na ndo kwaanza tukaonekana limbukeni...yani unavyozidi kumjali anazidi kukuumiza makusudi.Kiufupi inategemeana na mwanamke .

    JibuFuta
  5. Inategemea na mwanamke

    JibuFuta
  6. Kunadhana ya mwanamke kumfanyia mpenzi wake jambo la kumuumiza hasa kihisia kwalengo la kupima anapendwa kiasigani hii imekaaje mkuu

    JibuFuta
  7. Jina langu ni Ago, kutoka Albania. Nitapenda kushiriki uzoefu wangu juu ya jinsi ninavyopona mpenzi wangu mzuri kutoka kwa mnyang'anyi wa mke
    Nilipoteza rafiki yangu wa kike safi na mzuri kwa mtu mwingine. Nilikuwa na huzuni na nilitaka arudi vibaya tena. Nilikuwa nikimpigia Dk.Sango kwa usomaji na ushauri na nikagundua atanisaidia. Uchawi wake wa upatanisho ulimrudisha mpenzi wangu mpendwa. alisahau kabisa juu ya yule mtu mwingine na alirudi kwangu akiwa wazi na mwenye upendo kama hapo awali. Sasa wasiliana na daktari, Dk Sango, ikiwa unahitaji kushauri juu ya uhusiano wako au aina yoyote ya shida kwenye barua pepe yake. inaelezea mtaalam937@gmail.com

    JibuFuta
  8. Nilikuwa kwenye hatihati ya kumpoteza mke wangu wa miaka sita kwa sababu alisema hakuwa na hamu tena na ndoa yetu, ambayo inalea binti mzuri kwa sababu kama dereva wa lori huwa nikienda barabarani, lakini nampenda sana na namjali mke wangu. Nilimuuliza yeye na binti yangu shida ni nini, lakini hakutoa ufafanuzi mzuri, akisema alikuwa amechoka na umoja wetu, ilikuwa ya ajabu kwangu kwa sababu mke wangu alikuwa mwanamke mwenye upendo, ghafla kila kitu hubadilika tu. na mtazamo wake kwangu haukuwa mzuri, nilijua ilikuwa mbaya mahali pengine, kwa hivyo nilielezea mambo kwa rafiki yangu mzuri Micheal, ambaye alinitambulisha kwa jina la mwandishi wa spell Dr.Pellar, nilielezea hali yangu kwa mwandishi, ilifanya ninatambua kuwa mpenzi wa zamani alikuwa akimdanganya mke wangu kuniacha, lakini akaniambia nisiwe na wasiwasi. Nilifuata maagizo yote na mke wangu alirudi kwa ustawi wake wa kawaida na ninashukuru sana kwa kile msaidizi wa Dr.Pellar amenifanyia, kwa hivyo nashiriki shuhuda zangu ikiwa unakabiliwa na shida yoyote maishani na unahitaji suluhisho kuwasiliana na daktari huko DrPellar kwenye barua pepe yake drpelar@gmail.com

    JibuFuta
  9. da very nice class

    JibuFuta
  10. Sikuamini kuwa ningeweza kuungana tena na mpenzi wangu wa zamani, nilipatwa na kiwewe nikiwa nimesimama peke yangu bila mwili kusimama na mimi na kuwa nami, lakini nilipata bahati sana siku moja nilikutana na mchawi huyu wa hodari Dk. ASUBUHI, baada ya kumueleza hali yangu alifanya kila liwezekanalo kumuona mpenzi wangu anarudi kwangu, kweli baada ya kunifanyia uchawi mpenzi wangu wa zamani alirudi kwangu chini ya masaa 48, mpenzi wangu wa zamani alirudi akiniomba kuwa hatawahi. niache tena, miezi 3 baadaye tulioana na kuoana, ikiwa pia una hali sawa. Ana nguvu nyingi katika mambo yake;
    *penda uchawi
    * kama unataka ex wako nyuma
    * Acha talaka
    *kuvunja mawazo
    * huponya viharusi na magonjwa yote
    * uchawi wa ulinzi
    *Ugumba na matatizo ya ujauzito
    Wasiliana na Dk DAWN kwa barua pepe yake: dawnacuna314@gmail.com
    Whatsapp: +2349046229159

    JibuFuta
  11. Sikuamini kuwa ningeweza kuungana tena na mpenzi wangu wa zamani, nilipatwa na kiwewe cha kusimama peke yangu bila mwili wa kusimama na kuwa nami, lakini nilipata bahati sana siku moja nilikutana na Dk DAWN, baada ya kumwambia. kuhusu hali yangu alifanya kila liwezekanalo kumuona mpenzi wangu anarudi kwangu, kiukweli baada ya kunifanyia uchawi mpenzi wangu wa zamani alirudi kwangu chini ya masaa 48, mpenzi wangu wa zamani alirudi huku akiniomba kuwa hatoniacha kamwe. tena. Miezi 3 baadaye tulioana na kuoana, ikiwa una hali sawa. Ana nguvu nyingi katika mambo yake;
    * upendo
    inaelezea * inaelezea kivutio
    * kama unataka ex wako nyuma
    *acha talaka
    *kuvunja mawazo
    * huponya viharusi na magonjwa yote
    * uchawi wa kinga
    *Ugumba na matatizo ya ujauzito
    * bahati nasibu
    * bahati nzuri
    Wasiliana na Dk Ediomo kwenye barua pepe yake: dawnacuna314@gmail.com
    Whatsapp:+2349046229159

    JibuFuta
  12. kama ungependa kuokoa uhusiano/ndoa yako basi nitakupendekeza kwa Dk Dawn. alinisaidia kurejesha nyumba yangu baada ya miezi 11 ya utengano mkali kati yangu na mume wangu. Nilielekezwa kwake na dada yangu mkubwa wakati ndoa imeisha, akarudisha amani na furaha katika ndoa yangu, pia amesaidia marafiki zangu wengine na wanaishi kwa furaha kwa msaada wa Dk Dawn,
    Wasiliana naye ikiwa unahitaji usaidizi wa kurejesha uhusiano/ndoa yako/ ikiwa unataka kupata mimba au kuponya aina yoyote ya ugonjwa:
    Dk Dawn hatawahi kukukatisha tamaa:
    Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com
    WhatsApp: +2349046229159

    JibuFuta
  13. inatogel ยอดเยี่ยมเว็บที่เก็บรวบรวมเกมสล็อตพีจีออนไลน์ไว้อย่างแน่นและก็เป็นเว็บไซต์ที่มาแรงที่สุดของยุคนี้ pg slot เว็บไซต์ตรงไม่ผ่านเอเย่นต์ แจ็กพอเพียงตแตกมากมาย แตกจริง

    JibuFuta
  14. ทางเข้า pk789 สล็อต กำลังมองหาความสนุกในโลกของสล็อตออนไลน์? เรียนรู้ทุกสิ่งที่คุณต้องรู้เกี่ยวกับในคู่มือนี้ครบถ้วนและเต็มไปด้วยข้อมูลที่น่าเชื่อถือ PG รวมถึงเคล็ดลับสำหรับความสำเร็จ

    JibuFuta
  15. mind pg เว็บไซต์สล็อตลิขสิทธิ์แท้ พนันไม่ผ่านเอเย่นต์ ปากทางเข้าสู่เว็บไซต์สล็อตเจ้าใหญ่ของเมืองไทย เดี๋ยวเดียวที่จะพาท่านไปพบกับเกมหลายชนิด pgslot ความสนุกไม่มีใครเหมือน

    JibuFuta
  16. เว็บสล็อต pg ทั้งหมดฟรี ที่ดีที่สุดที่เสนอเกมสล็อตฟรีมากมาย สำรวจโลกของเกมสล็อตฟรีและเรียนรู้วิธีการค้นหาแพลตฟอร์มที่ PG SLOT น่าเชื่อถือเพื่อเพลิดเพลินกับประสบการณ์เล่นสล็อตที่น่าตื่นเต้นโดยไม่ต้องใช้เงินใด

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Zilisomwa zaidi wiki hii...

Maana ya Saikolojia na Nafasi Yake Katika Jamii -1

Pay $900? I quit blogging

Haiba ni nini?

Heri ya mwezi mpya!