Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Vipaumbele

Vitabu Nilivyosoma kwa Mwaka 2017!

Picha

Namna ya Kuutambua Wito wa Maisha Yako

Picha
PICHA: B aha'i Blog Umewahi kufanya kazi zenye heshima lakini hujisikii ridhiko ndani yako? Unapata kipato kizuri na watu wengine wanatamani kufanya unachokifanya lakini wewe mwenyewe hufurahii.  Unakuta umesoma vizuri lakini huoni thamani ya kile ulichokisoma. Zaidi ya kutaja chuo ulichosoma na ngazi ya elimu uliyofikia huoni namna gani elimu yako inakusaidia kutoa mchango kwa jamii.

Wajibu wa Wamiliki wa Shule za Msingi za Bweni

Picha
PICHA: B ORGEN Magazine TUMESHAURIANA mambo kadhaa ya kuzingatia tunapolazimika kuwapeleka watoto wadogo kwenye shule za msingi za bweni. Kubwa zaidi ni mzazi kujiridhisha na namna shule inavyomwekea mtoto mazingira mazuri yanayofanana na yale ya nyumbani.

Unavyoweza Kutumia Mshahara Kujikwamua Kiuchumi

Picha
Wapo watu wanawakejeli wafanyakazi kwa kuajiriwa. Kwamba kama mtu asiye na elimu anaweza ‘kuosha magari mtaani’ na akakuzidi kipato kuna sababu gani kuishi maisha magumu ofisini? Upo ukweli wa namna fulani. Wafanyakazi wengi wanaishi maisha ya ukata. Kazi yao kubwa ni kupambana kuhakikisha kuwa mishahara inakutana. Katika mazingira ya namna hii, inakuwa vigumu kupiga hatua za maana kimaisha.

Tabia Saba Zitakazokuwezesha Kutekeleza Malengo Unayojiwekea

Picha
KUANZA kwa mwaka mpya kunaambatana na matarajio mengi. Tunapoingia mwaka mpya tunamani kubadili maeneo mengi katika maisha yetu. Tunatamani kuwa na maisha bora yenye tija kiuchumi, kijamii, kiimani na kwenye maeneo mengine. Hata hivyo, katika kutekeleza malengo yako, ni dhahiri kuwa zipo baadhi ya tabia ulizonazo zinazoweza kuwa kikwazo katika kutekeleza malengo ya mwaka huu. Unahitaji kubadili tabia ili uweze kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kutekeleza malengo yako.

Vitabu 49 Nilivyovisoma Mwaka 2016

Picha
Namshukuru Mungu nimeweza kusoma vitabu 49 kwa mwaka 2016. Nimejifunza mengi. Kusoma ni kama kupata nafasi ya kufanya mazungumzo na watu wa kila namna ya uelewa ambao kwa hali ya kawaida usingeweza kuwasikia vijiweni.  Msisitizo wangu umekuwa kwenye vitabu vinavyochambua tabia katika maeneo mbalimbali ya maisha. Hata hivyo, vipo vichache vya masuala ya imani, falsafa na dini. Sijawa msomaji wa riwaya/novel. Nikutie moyo wewe mwenye ratiba ngumu kwa siku. Unaweza kufanya maamuzi ya kusoma ikiwa utaamua kuweka ratiba yako vizuri. Nijitolee mfano mimi mwenyewe.

Siri za Watu Wanaotekeleza Maazimio ya Mwaka Mpya

Picha
TULIJADILI baadhi ya sababu zinazofanya watu washindwe kutekeleza maazimio wanayoyaweka kila mwaka mpya unapoanza. Tuliona sababu kubwa tatu; kuweka maazimio kwa msisimko tu wa kuingia mwaka mpya usioenda sambamba na tafakari ya kina; kuweka malengo mapana mno yasiyopimika; na pale malengo yanapohusisha mabadiliko ya tabia, kutokujua uliko mzizi wa mabadiliko hayo.

Kwa Nini Maazimio Mengi ya Mwisho wa Mwaka Huwa Hayatekelezeki?

Picha
Kila mwaka mpya unapoanza, ni kawaida kwa watu wengi kuweka maazimio fulani ya kutekeleza. Wapo ambao huazimia kubadili tabia wasizozipenda. Wengine huazimia kuanzisha mwenendo mpya wa maisha wanayoyatamani. Wengine hufikiria kutekeleza malengo fulani ya kijamii na kiuchumi yatakayobadili maisha yao kwa mwaka unaoanza. Ingawa ukweli ni kuwa mwaka unapoanza kinachobadilika huwa ni tarehe tu, watu huwa na imani kuwa wanaingia kwenye zama za maisha mapya. Imani hiyo huambatana na jitihada za kujaribu kubadili maisha yao yaendane na zama hizo mpya. Wanasema, ‘mwaka mpya na mambo mapya!’

Jinsi ya Kumsaidia Mtoto Anayefanya Vibaya Shuleni

Picha
Si jambo la kufurahisha kwa mzazi unapoona mtoto hajafanya vizuri masomoni. Unapofahamu kuwa maendeleo ya mwanao si kama vile ulivyotarajia, ni rahisi kupatwa na simanzi, wasiwasi na hasira. Ni dhahiri mzazi unatamani mtoto awe na mustakabali mzuri kimaisha. Matumaini hayo yanakufanya uchukulie kushindwa kwake masomo kama kiashiria cha kuharibika kwa maisha yake ya baadae. Hakuna mzazi angependa mtoto awe na maisha yasiyoeleweka.

Mbinu za Kutafuta Ajira Mtandaoni

Picha
Changamoto kubwa inayoweza kukukabili unapotafuta kazi, ni taarifa zitakazokusaidia kujua uelekeze wapi maombi ya kazi. Zamani, ili kupata taarifa za kazi, watu walitegemea radio, magazeti, televisheni na taarifa za marafiki wanaofahamiana nao. Mambo yanazidi kubadilika kwa kasi. Sasa hivi, kwa mfano, matumizi ya mtandao yamerahisisha namna tunavyoweza kupata taarifa hizi. Hata hivyo, pamoja na uwepo wa mtandao, bado kuna changamoto ya wapi hasa waweza kupata taarifa sahihi. Mbinu zifuatazo ni matokeo ya uchambuzi wa tafiti mbalimbali na zinaweza kukupunguzia changamoto ya kupoteza muda na nguvu nyingi kutafuta kazi mtandaoni.

Mambo Matano Yanayoweza Kukusaidia Kupata Muda wa Kuwa Karibu na Mtoto

Picha
Wazazi wengi wanapenda kuwa karibu na watoto  kwa lengo la kuwajengea mazingira ya kujifunza. Changamoto, hata hivyo, ni kukosa muda wa kutosha kufanya hivyo. Kwa mfano, ni kawaida kwa wazazi kutoka nyumbani alfajiri na kurudi usiku wakati ambao tayari watoto wameshalala. Matarajio makubwa ya kikazi yamekuwa kipaumbele na hivyo tunatumia muda mwingi kufanya kazi ambazo kimsingi ndizo zinazotusaidia kuwatunza watoto wetu.  Hata hivyo, majukumu  yetu haya muhimu yanatufanya wakati mwingine tukose muda wa kuwasaidia watoto kihisia, kiufahamu na hata kimahusiano kama tunavyotamani. Makala haya yanajadili hatua tano za kuchukua ili kukusaidia mzazi kupata muda wa kuwekeza katika malezi ya watoto wako.

Mambo Sita ya Kufanya Unapotafuta Kazi

Picha
Kutafuta kazi ni kuingia kwenye soko la ajira ambalo kimsingi ni uwanja unaowakutanisha watu wenye mahitaji makubwa ya aina mbili. Upande mmoja, wapo watu wenye ‘bidhaa’ ya ujuzi na weledi, lakini wenye hitaji la kujipatia kipato kwa kutumia ujuzi na maarifa waliyonayo. Hawa wanaitwa watafuta kazi.

Wajibu wa Mzazi Kama Mwalimu wa Kwanza wa Mtoto

Picha
Tafiti nyingi za mazingira ya kujifunzia zimeendelea kusisitiza kuwa elimu bora kwa mtoto huanzia nyumbani. Kuwepo kwa mazingira rafiki ya kielimu nyumbani kunampa mtoto nafasi ya  kukua kiufahamu na humuandaa vyema kujifunza kabla hajaanza shule rasmi. Kimsingi, mzazi ndiye mwalimu wa kwanza anayemwezesha mtoto kujifunza vizuri. Mtoto hujifunza kutembea, kuongea, kujilisha, kazi za nyumbani na kadhalika kwa msaada wa mzazi. Ikiwa mzazi atatambua wajibu wake kama mwalimu wa mtoto na akautekeleza ipasavyo, kazi ya mwalimu shuleni hurahisishwa.

Mwaka Mmoja Bila Mama, Mkono wa Mungu Haujatuacha…

Picha
Nakumbuka mwezi Juni 2002, nikiwa mwanafunzi wa sekondari, eneo ni stesheni ya gari moshi (treni) mjini Singida nikiwa ninarudi nyumbani nikitokea Dodoma. Ilikuwa ni safari ya kuunga unga iliyoanzia Dar es Salaam kupitia Dodoma na kisha Singida. Wakati huo tulikuwa tunaondoka Dodoma saa nne asubuhi, Singida tunafika saa za jioni kuanzia saa kumi na moja hivi tukiwa taabani kwa uchovu wa kukaa kwenye mabehewa yaliyoonekana kuhangaika mno kupita kwenye mataruma katikati ya vichaka ya Dodoma na Singida. Jioni hiyo ninayoikumbuka vyema tulichelewa kidogo na hatimaye tulifika Singida stesheni saa kumi na mbili unusu hivi za jioni.

Kuanzisha na Kuimarisha Urafiki wa Karibu

Picha
Katika zama hizi za maendeleo ya kidijitali, ni rahisi sana kufahamiana na watu wengi ambao, hata hivyo, wanaweza wasiwe marafiki. Unaweza, kwa mfano, kuwa na ‘marafiki’ elfu tano kwenye mitandao ya kijamii, lakini usiwe na rafiki hata mmoja katika maisha halisi. Marafiki wa kweli na wa karibu ni moja wapo ya mahitaji muhimu katika maisha. Tunaweza kuwa na sababu nyingi kuhalalisha kwa nini hatuna (haja na) marafiki wa karibu.  Hata hivyo, zipo nyakati  hufika tukajikuta katika maisha yenye kujaa upweke  na msongo wa mawazo kwa sababu hatukutumia muda wetu kutengeneza urafiki wa karibu na watu tunaofahamiana nao.

Umuhimu wa Kujenga Tabia ya Kujitolea

Picha
Kujitolea ni kutoa sehemu ya muda wako, ujuzi na maarifa uliyonayo na wakati mwingine nguvu zako kufanya kazi ya watu wengine bila kupata malipo ya moja kwa moja. Kazi unayoifanya kwa kujitolea mara nyingi ungeweza kuifanya kwa kudai ujira lakini unaamua kuifanya bure.  Mathalani, mwajiriwa anayetamani kuleta mabadiliko nje ya ajira yake, anapotumia ujuzi wake kufanya kazi za jamii bila kudai malipo, anakuwa amejitolea. Tuangalie kwa mhutasari kwa nini ni muhimu kujenga tabia ya kujitolea.

Makundi Manne ya Tabia za Watoto Kitabia

Picha
Ingawa ni kweli tunazaliwa na sehemu ya tabia tulizonazo, upo ukweli wa kiutafiti unaothibitisha kwamba mazingira ya kimalezi yana nafasi kubwa katika kujenga tabia za mtu. Ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili, mathalani, unatawaliwa zaidi na uasili ambao kwa kiasi kubwa hatuna mamlaka nao. Hata hivyo, ukuaji wa kihisia na kimahusiano unatawaliwa zaidi na mazingira ya kimalezi ambayo tayari tuliyaona kwenye makala iliyopita .

Miaka miwili ya Kuwa 'Mama' Ina Mafunzo Makubwa Kwangu...

Picha
Nilipoamua kuchukua uamuzi wa kubadilishana majukumu na mke wangu sikujua ni kwa jinsi gani uamuzi huo ungenibadilisha mimi na kunipa mtazamo mpya kabisa katika maisha. Baada ya kuzaliwa Baraka siku kama ya leo mwaka 2012 tuliamua kubadilishana majukumu ya familia; mimi nibaki na kuangalia watoto na kutunza nyumba na mahitaji yake yote na mke wangu aendelee kufanya kazi na kusaidia wakati wowote anaoweza.

Umuhimu wa kutofautiana ili kujenga mahusiano imara

Picha
Kwa wale wafuatiliaji wenzangu wa tamthlia isiyopendwa na wengi, Isidingo the Need, mtakuwa mmeona mgogoro wa kimahusiano kati ya Rajesh Kumar na mkewe Priya. Wawili hawa wamejaliwa mtoto mmoja wa kike, Hiranya, ambaye si mtoto wa kuzaa wa Rajesh. Sasa ikafika mahali mwanaume huyu akatamani kuwa na mtoto ‘wa kumzaa mwenyewe’. Priya hayuko tayari kupata mtoto mwingine. Anadhani   kilicho muhimu kwa sasa ni kumlea mtoto wao na sio kuongeza majukumu ya malezi.

Shukrani za pekee kwa Prof. Mbele kwa zawadi ya thamani!

Picha
'Africans and Americans Embracing Cultural Difference', ni kitabu kizuri nilichokisoma kwa mara ya kwanza Aprili, 2009 nilipokiona katika duka la vitabu KIMAHAMA, Arusha. Ilikuwa ni baada ya kukisikia kikisemwa na rafiki yangu mmoja. Ni miaka mitano imepita, lakini kitabu hiki hakikuwahi kuizoea maktaba yangu tangu wakati huo. Kusoma kitabu chenye saini ya mwandishi, si jambo linalowatokea wengi. Ni muujiza ulionitokea. Picha: Jielewe Kwanza, kwa rafiki zangu wasomaji waliofika kwangu kwa mazungumzo ya vitabu na waandishi, kitabu hiki hakikukosekana kwenye mazungumzo hayo. Na kila aliyesikia sifa zake, alipenda kuthibitisha ikiwa nilisema  kweli kwa kukiazima. Kiliazimwa na wasomi, wasafiri, waongozaji wa watalii (tour guide), wapenda maarifa, kutaja kwa uchache. Ni bahati mbaya sana kwamba hakikuwa kinapatikana katika baadhi ya maeneo. Hivyo, kiliazimwa, na kuazimwa, tena na tena kwa muda wa miaka miwili. Mwaka 2011, kiliondoka rasmi kwenye maktaba yangu. Nilikuja k...