Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Vituo vya Malezi

Tutafakari hatari ya ‘malezi ya bweni’

Picha
PICHA:  Aparna Wazazi hawaamui tu kuwapeleka watoto wadogo kusoma shule za msingi za bweni. Ukiwasikiliza, mara nyingi wanakuwa na sababu za msingi kufanya maamuzi hayo magumu. Masuala kama migogoro ya kifamilia, wazazi kutokupatikana nyumbani, kutokuaminika kwa walezi mbadala mfano, wadada wa kazi, ni baadhi ya sababu zinazowafanya wazazi waamue kulipa gharama kubwa ya kuwakabidhi watoto kwa walezi wanaoaminika shuleni. Nafahamu wapo wazazi wanaochukulia shule za bweni kama sehemu ya kuonesha uwezo wao wa kifedha. Kwa mfano, baadhi ya wazazi hususani wale wenye uwezo wa kifedha, huzifikiri namna nzuri ya kuonesha ‘kujali elimu ya mtoto’ ni kumpeleka kwenye shule ya gharama kubwa na hata ikibidi shule ya msingi ya bweni ‘ili mtoto akazingatie masomo na apate muda wa kutulia.’ Hawa ni wachache lakini wapo. Shule pia zinazowaaminisha wazazi kuwa taaluma inapatikana bweni nazo zipo. Saa nyingine ni mchanganyiko wa nia njema, biashara au basi tu kukosa uelewa. Ukweli unabaki kwamb...

Madhara ya Kumpeleka Mtoto Shule ya Bweni

Picha
PICHA: Daily Maverick Moja wapo ya sababu nyingi zinazowasukuma wazazi kuwapeleka watoto wadogo kusoma shule za bweni ni mafanikio ya taaluma. Mazingira ya shule yanaaminiwa kuwa bora zaidi katika kuwasaidia watoto kufanya vizuri zaidi kuliko wanapokuwa nyumbani.

Je, Shule za Bweni Zinafaa kwa Malezi ya Watoto Wadogo?

Picha
PICHA: SOS Schools Ongezeko kubwa la shule za bweni kwa watoto wadogo ni kiashiria kimoja wapo cha mabadiliko ya kijamii yanayoendelea kuathiri desturi za malezi. Pamoja na changamoto zake, mzazi anapofanya maamuzi ya kumpeleka mwanae shule ya bweni huamini anafanya hivyo kwa faida ya mtoto.

Kwa nini Wazazi Huwapeleka Watoto Wadogo Shule za Bweni?

Picha
PICHA: The Citizen Miaka kadhaa iliyopita, wakati huo nikiwa mwanafunzi, nilishangazwa kusikia mtoto wa ndugu yangu, wakati huo akiwa na miaka sita, alikuwa anasoma shule ya bweni. Sikufikiri jambo hilo lingewezekana.                                                                                     Nakumbuka mara yangu ya kwanza kwenda shule ya bweni nilikuwa na umri wa miaka 17 nikisoma kidato cha 5. Kwa kuwa haikuwa rahisi kwangu kuzoea maisha ya mbali na nyumbani, nilishindwa kuelewa inawezekanaje mzazi kumpeleka mtoto mdogo kiasi hicho kwenda shule ya bweni.

Tunavyoweza Kuboresha Vituo vya Malezi

Picha
PICHA: John-Paul Iwuoha MALEZI katika vituo vya kulelea watoto hayakwepeki. Katika mazingira ambayo wazazi wanafanya shughuli zao mbali na nyumbani kituo cha malezi kinakuwa msaada. Tafiti za malezi zimekuwa zikijaribu kuangalia namna gani huduma hizi zinavyoweza kuboreshwa. Moja wapo ya mashirika maarufu katika eneo hili ni   Taasisi ya Marekani ya Mtandao wa Afya ya Mtoto na Maendeleo ya Utafiti wa Malezi ya Watoto (NICHD) .

Unayopaswa Kuzingatia Unapompeleka Mtoto Wako Katika Vituo vya Malezi -1

Picha
PICHA: Hope for Bukasa UTARATIBU wa wazazi kuwapeleka watoto kwenye vituo vya malezi umeanza kuwa maarufu hapa nchini. Karibu kila mji mdogo katika mikoa yote vipo vituo kadhaa mahususi kwa ajili ya kuwatunza watoto wakati wazazi wao wakiwa kazini. Kinachofanya huduma ya malezi ya vituoni kuwa maarufu ni changamoto za akina dada wa kazi, ambao mara nyingi, huwa ni wadogo kiumri na hawana uwezo wala ari ya kuwalea watoto vizuri.

Wajibu wa Wamiliki wa Shule za Msingi za Bweni

Picha
PICHA: B ORGEN Magazine TUMESHAURIANA mambo kadhaa ya kuzingatia tunapolazimika kuwapeleka watoto wadogo kwenye shule za msingi za bweni. Kubwa zaidi ni mzazi kujiridhisha na namna shule inavyomwekea mtoto mazingira mazuri yanayofanana na yale ya nyumbani.

Mzazi Ufanyeje Unapompeleka Mwanao Shule ya Bweni?

Picha
PICHA: Paul Jeffrey PAMOJA na changamoto za malezi ya shule za bweni tulizoziona, bado mzazi anaweza kulazimika kumpeleka mwanae kwenye shule hizi. Kwanza, kuna suala la kazi. Wazazi wanaofanya kazi mbali na familia zao wanaweza kuamua kuwapeleka watoto kwenye shule ya bweni ili wasiwe na wasiwasi na uangalizi wao.

Namna Shule za Msingi za Bweni Zinavyoathiri Tabia za Watoto -3

Picha
KATIKA makala yaliyopita, tumeona kuwa shule za msingi za bweni zinachangia kuwanyima watoto fursa ya kujifunza ujuzi wa kujitegemea. Uwezo hafifu wa kujifunza stadi za maisha, kwa kiasi kikubwa, unachangiwa na matarajio makubwa ya kitaaluma waliyonayo wazazi kwa watoto wao. Wamiliki na waendeshaji wa shule za bweni, kimsingi, wanaitikia wito wa wazazi wanaotarajia watoto wao kujifunza maarifa ya shule zaidi hata ikibidi kwa gharama ya kudumaza maeneo mengine muhimu ya kimakuzi.

Tunayopaswa Kuyafahamu Kuhusu Shule za Msingi za Bweni -2

Picha
Tulianza kujadili namna gani mazingira ya shule za bweni yanavyochangia kuwasaidia watoto wadogo kuimarika kiakili. Bonyeza hapa kama hukusoma makala hiyo. Tuliona shule za bweni zinaweka mazingira sisimushi yanayowajenga watoto kiufahamu zaidi kuliko wenzao wanaoishi nyumbani. Mambo kadhaa yanaonekana kuchangia kukuza uwezo huu. Kwanza, tulitaja uwepo wa ratiba inayoongoza mtiririko wa shughuli za watoto wanapokuwa katika mazingira ya shule.

Tunayopaswa Kuyafahamu Kuhusu Shule za Msingi za Bweni

Picha
Katika miaka ya hivi karibuni, shule za msingi za bweni zimekuwa maarufu. Kimsingi, si tu shule za msingi, lakini hata shule za awali za bweni. Hivi sasa, miji karibu yote katika nchi hii inazo shule kadhaa zinazopokea watoto wadogo na kuwasomesha kwa mfumo wa bweni. Takwimu rasmi za hivi karibuni hazipatikani. Lakini kwa mujibu wa Wizara ya Elimu, mwaka 2012 nchi yetu ilikuwa na shule za msingi zipatazo 684 zenye huduma ya bweni. Shule hizi zinafahamika pia kama shule zinazotumia Kiingereza kama lugha rasmi ya kufundishia, yaani English Medium, zikimilikiwa na watu binafsi au taasisi zisizo za umma.

Mambo ya Kuzingatia Unapompeleka Mwanao Kwenye Kituo Cha Malezi

Picha
Watafiti wa malezi ya watoto wamejaribu kuangalia namna gani huduma za malezi ya kituoni –day care yanavyoweza kuboreshwa. Moja wapo ya watafiti maarufu katika eneo hili ni   Taasisi ya Marekani ya Mtandao wa Afya ya Mtoto na Maendeleo ya Utafiti wa Malezi ya Watoto (NICHD) . Maswali ya msingi yanayojaribu kujibiwa na tafiti hizi ni ikiwa kuna uhusiano wa ubora wa huduma zinazotolewa na vituo hivi na makuzi ya mtoto katika nyanja za kiakili, kihisia, kimwili na kistadi; aina ya mazingira yanayoweza kuhusianishwa na ukuaji mzuri wa kihisia na kiakili kwa mtoto na kiasi cha masaa kinachopendekezwa kwa mtoto kulelewa katika kituo kwa siku/juma.