Jana nilikuwa nikitazama kipindi cha kiislamu kwenye televisheni ya Chaneli 10. Suala la mali katika ndoa za dini hiyo lilikuwa likijadiliwa. Kwamba Kiislam, mali katika ndoa si suala la wanandoa kwa pamoja. Kwamba mali anazoingia nazo mwanandoa kwenye ndoa, zinabaki kuwa zake mwenyewe. Na wakiachana, kila mmoja anaondoka na alichokuja nacho. Hata ndani ya ndoa, mali zinapatikana 'separately' kwa maana ya kwamba kila anachopata mwanandoa hicho ni haki yake yeye mwenyewe. Wakitengana, kila mtu anaondoka na vyake. Katika kufakari hayo, nilijaribu kumfikiria mwanamke na nafasi yake katika ndoa. Nikamwona kama kiumbe anayenyanyaswa na dini. Kwa nini? Wanaume wengi hutafuta mali kwanza ndio waoe, na hata wanapooa, huwaoa wanawake watakaowategemea wao. Katika hali hii nini salama ya mwanamke katika dini inayoruhusu talaka? Hizi si dalili za wazi za ukandamizaji wa jinsia ya kike?
Hiki ndio kwanza nakisikia hapa. Huenda tuko wengi. Shukrani kwa kutuongezea upeo.
JibuFutaHata mimi sijakisoma, labda tukitafute...!
JibuFutamie nimekisoma. Nilikipata Machi 09 mwaka jana hapa hapa jijini Dar.
JibuFutaMie niliwahi kukisikia lakini sijawahi kukiweka machoni!:-(
JibuFutaVipi kinaeleweka au mambo zake kwa mbongo ni alinacha?
@Fadhy: Aliekisoma anasemaje, Wenzetu? Kweli tutatajirika tukikisoma? Au tutakuwa Shetani kabisa? Maana yake hua nikisoma vitabu vya dini fulani "Babylon" inafananishwa na sehemu au ulimwengu wenye dhambi zote.
JibuFutaNinachokifurahia hapa ni kwamba niko katika kundi la akinaProf Mbele, Simon Kitururu, M3 na wengine kabisa (MEN AND WOMEN OF LETTERS) ambalo BADO TU KuSOMA KITABU HICHO!
Nasema "kifo cha wengi harusi".