Kama sio utumwa ni nini hiki?
Habari za siku ndugu msomaji. Binafsi sijambo. Nafurahi kurejea kibarazani baada ya heka heka za huko na huko. Itoshe kuhusu mimi, nikukaribishe tena humu ndani. Leo ningependa kukusimulia kisa kimoja. Nikuase kwanza, kwamba usilazimike kunielewa vibaya. Sijawa na tabia ya kuona makosa zaidi niwapo mahali ama nikutanapo na watu. Maana siamini kwamba binadamu ana kazi ya kushabikia makosa kuliko jema moja. Nisijitetee sana. Jumapili hii nilipata fursa ya kuhudhuria ibada kwenye kanisa la 'kisomi'. Washirika wa kanisa hili, wengi wao ni wale ambao umande haukuwazuia kuhudhuria shule. Wamesoma. Pamoja na ukweli kwamba wote walikuwa weusi kama mimi, lakini ilikuwa bayana kwamba kiingereza kilikuwa 'nguzo' ya ibada hiyo. Hilo halikuwa tatizo kwangu. Maana inaeleweka kwa wengi wetu kwamba, kusoma kunathibitishwa na umahiri wa kusema kiingereza. Nshazoea hili. Pamoja na ukweli kwamba kiuhalisia kiswahili ndicho kinachotawala madarasani lakini watu hatutaki kuukubali ukweli...

hahahaha kazi kwelikweli!
JibuFutaUnafikiri yaani ni kaaaaziii kwelilweli:-)
JibuFutaMwanzo mgumu, siyo? Hasa katika masuala ya UJAMAA!
JibuFutaLabda tuchunguze zaidi kuhusu jinsi tunavyohusiana na hao ndugu zetu: wakoloni wa kale kama Wingereza, Ujerumani na wenginevyo.
Maana yake huwezi ukiwa CCM ukaendesha kwa mafanikio siasa za ujamaa na kujitegemea wakati huku unaendelea kufurahia "msaada" kutoka nchini za mabepari hususan zile ambazo ziliyekuwa zinamkandamiza Mwafrika enzi za ukoloni.
Suali kwenu Mabwana Fede na Bwaya:
"Je, tunapata mafunzo gani kutoka huko Zimbabwe?"
http://news.xinhuanet.com/english2010/china/2011-02/12/c_13728225.htm
sasa hapa kilipo chama tajwa kipo katika hatua ipi kati ya hizo hapa juu?
JibuFutaHa ha ha haaa , utani mwingine bwana!!!
JibuFutanice blog
JibuFutathanks you for sharing
JibuFutai like it this blog
JibuFuta