Uwongo unalipa sio?

Kwa jinsi ambavyo kujielewa ni kazi nzito, waungwana tuko tayari tuambiwe uwongo tufurahi, turidhike.

Kuliko tunaambiwe ukweli unaouma, uwezao kutubadilisha.

Kwa maana nyingine tunafanya bidii kusikia tunachotaka kusikia.

Maoni

  1. kaka Bwaya, hapa kazi hipo.Darasa kali, kazi kwelikweli

    JibuFuta
  2. Ukweli ndiyo huo,jamii imetufundisha kuukubali uongo ili tujisikie nafuu.
    Kaka bwaya kuna kitu ninajiuliza ni kwanini tulipokuwa wadogo tuliambiwa kumpa mtu kitu kwa mkono wa kushoto ni kukosa adabu?Wanablog naomba msaada wenu?

    JibuFuta
  3. Kweli kabisa,Ndg Bwaya.Ndio maana baadhi ya watawala wanachotaraji katika hotuba zao ni makofi,vigeregere,shwangwe,vifijo,nderemo,makofi,nk...akizomewa,basi hapo hapakaliki.

    JibuFuta
  4. Tatizo kubwa ni kwamba tukiambiwa ukweli huwa tunakasirika na kuwa wakali, lakini pamoja na hayo mi bado napenda kuambiwa ukweli ila tu uwe kwenye soft language kidogo

    JibuFuta
  5. Yule bwana aliyewahi kusema kuwa dunia hii ina umbo la bapa kama meza alionekana mkweli, lakini yule aliyesema kuwa dunia ina umbo la duara aliswekwa lupango kwa na mfalme kwa kusema uongo.

    kaka Bwaya leo hii ukisema kuwa njia hii ya kuchagua viongozi wetu kwa kutumia nadharia ya Wagiriki wenyewe wanaita Demokrasia haitufai bali turejee kwenye zile njia zetu za asili za kuwapata viongozi walizotumia mababu zetu utaonekana mwehu na juha.

    JibuFuta
  6. Habari za hapa Kaka Bwaya.

    Nimepita hapa kibarazani kwako kujitambulisha kuwa nimefungua kijibaraza changu kitakachokuwa kikijihusisha zaidi na masuala ya vijana.
    Nimekuwa nimsomaji wa blog yako kwa muda mrefu, na sasa nimeamua na mimi nijitose uwanjani ili kuongeza mchango katika kuielimisha jamii.
    Niko ntayari kuelimishwa na kukosolewa pale nitakapoonekana natoka nje ya mstari.
    Natarajia ushirikiano wako.

    Digna

    JibuFuta
  7. Bennet na Digna karibuni sana. Nafurahi kuwapokea kama wadau muhimu wa kibaraza hiki.

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Zilisomwa zaidi wiki hii...

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke-1

Maana ya Saikolojia na Nafasi Yake Katika Jamii -1

Haiba ni nini?

Tabia za Mtoto wa Miaka 0 – 3 Kimahusiano na Kihisia

Pay $900? I quit blogging