Kuna wakati unaweza kufikiri unaigiza msimamo na kejeli kwa maumivu ya mtu, unakuwa na maoni yasiyo na haya kwa mateso ya wenzako ukijua unawafurahisha watu fulani lakini hayo maigizo ya kukosa huruma kwa mwenzako yana uwezekano wa kugeuka tabia kweli na ukawa mtu katili kweli kweli. Michezo, dini na siasa visikuchochee kujiona una haki ya kubeza masaibu wanayopitia wenzako kwa sababu mdogo mdogo mizaha hugeuka ukweli. Mwaka 1971, Philip Zimbardo, mshunuzi na mwalimu wa Chuo Kikuu cha Stanford, alifanya utafiti maarufu kama #StanfordPrisonExperiment akilenga kuchunguza nguvu ya mazingira kwenye tabia. Utafiti ulivyofanyika Zimbardo alitengeneza gereza la kuigiza hapo chuoni likiwa na seli, mahali mfungwa angekaa mwenyewe, mahali pa wanyarapa kuishi, mahali wafungwa wangetoka na kuteswa na wanyapara. Washiriki walifanyiwa mchujo wa haiba kuona kama ni watu wenye utimamu wa tabia na hisia. Kwa njia ya nasibu (random assignment) wanafunzi...
kaka Bwaya, hapa kazi hipo.Darasa kali, kazi kwelikweli
JibuFutaUkweli ndiyo huo,jamii imetufundisha kuukubali uongo ili tujisikie nafuu.
JibuFutaKaka bwaya kuna kitu ninajiuliza ni kwanini tulipokuwa wadogo tuliambiwa kumpa mtu kitu kwa mkono wa kushoto ni kukosa adabu?Wanablog naomba msaada wenu?
Kweli kabisa,Ndg Bwaya.Ndio maana baadhi ya watawala wanachotaraji katika hotuba zao ni makofi,vigeregere,shwangwe,vifijo,nderemo,makofi,nk...akizomewa,basi hapo hapakaliki.
JibuFutaTatizo kubwa ni kwamba tukiambiwa ukweli huwa tunakasirika na kuwa wakali, lakini pamoja na hayo mi bado napenda kuambiwa ukweli ila tu uwe kwenye soft language kidogo
JibuFutaYule bwana aliyewahi kusema kuwa dunia hii ina umbo la bapa kama meza alionekana mkweli, lakini yule aliyesema kuwa dunia ina umbo la duara aliswekwa lupango kwa na mfalme kwa kusema uongo.
JibuFutakaka Bwaya leo hii ukisema kuwa njia hii ya kuchagua viongozi wetu kwa kutumia nadharia ya Wagiriki wenyewe wanaita Demokrasia haitufai bali turejee kwenye zile njia zetu za asili za kuwapata viongozi walizotumia mababu zetu utaonekana mwehu na juha.
Habari za hapa Kaka Bwaya.
JibuFutaNimepita hapa kibarazani kwako kujitambulisha kuwa nimefungua kijibaraza changu kitakachokuwa kikijihusisha zaidi na masuala ya vijana.
Nimekuwa nimsomaji wa blog yako kwa muda mrefu, na sasa nimeamua na mimi nijitose uwanjani ili kuongeza mchango katika kuielimisha jamii.
Niko ntayari kuelimishwa na kukosolewa pale nitakapoonekana natoka nje ya mstari.
Natarajia ushirikiano wako.
Digna
Bennet na Digna karibuni sana. Nafurahi kuwapokea kama wadau muhimu wa kibaraza hiki.
JibuFuta