Kuna wakati unaweza kufikiri unaigiza msimamo na kejeli kwa maumivu ya mtu, unakuwa na maoni yasiyo na haya kwa mateso ya wenzako ukijua unawafurahisha watu fulani lakini hayo maigizo ya kukosa huruma kwa mwenzako yana uwezekano wa kugeuka tabia kweli na ukawa mtu katili kweli kweli. Michezo, dini na siasa visikuchochee kujiona una haki ya kubeza masaibu wanayopitia wenzako kwa sababu mdogo mdogo mizaha hugeuka ukweli. Mwaka 1971, Philip Zimbardo, mshunuzi na mwalimu wa Chuo Kikuu cha Stanford, alifanya utafiti maarufu kama #StanfordPrisonExperiment akilenga kuchunguza nguvu ya mazingira kwenye tabia. Utafiti ulivyofanyika Zimbardo alitengeneza gereza la kuigiza hapo chuoni likiwa na seli, mahali mfungwa angekaa mwenyewe, mahali pa wanyarapa kuishi, mahali wafungwa wangetoka na kuteswa na wanyapara. Washiriki walifanyiwa mchujo wa haiba kuona kama ni watu wenye utimamu wa tabia na hisia. Kwa njia ya nasibu (random assignment) wanafunzi...
DUH! UMEBADILISHA KICHWA CHA HABARI?
JibuFutaAU.......
La kuvunda halina ubani!
JibuFutaUtalipatia ubani gani la kuvunda? Llikishavunda harufu yake ndo marashi yake tena.
Koero, sijabadili. Pengine ni kwa sababu nimepost zote na hiyo ya juu kwa muda unaokaribiana!
JibuFutaSubi, labda tuliweke kwenye jokofu, waonaje?
La kuvunda halina ubani, kifo hakina kinga,
JibuFutala kuvunda! Hata ukiliweka kwenye jokofu , litavunda tu, la kuvunda, hata kama sio leo, wala kesho, hata mtondo go, iko siku litavunda tu, kuliweka jokofuni, waliongezea tu siku za kutovunda! lakini litavunda tu.
La Kuvunda halina ubani
JibuFuta