PICHA: Shutterstock Katika makala yaliyopita tuliona mbinu tatu unazoweza kuzitumia kuelewa mambo unayojifunza. Kwanza, ni ‘njaa’ inayokusukuma kuelewa. Unapokuwa na ari ya kuelewa jambo, mara nyingi, utahamasika kulielewa bila kutumia nguvu nyingi. Pili, tuliona ni muhimu kutengeneza picha kubwa ya jambo unalojifunza kabla hujaanza kujifunza undani wa mambo madogo madogo ndani ya picha hiyo. Kwa mfano, unaposoma aina za vyakula, lazima kwanza uelewe vyakula. Uelewa wa jumla wa vyakula utakurahisishia kazi ya kuchanganua aina zake kwa sababu tayari unayo rejea utakayoitumia kuelewa zaidi. Mbinu ya tatu ni kukihusisha kitu unachokisoma na mambo unayoyafahamu tayari. Unaposoma aina za vyakula, kwa mfano, lazima uwe unafikiria vyakula mbalimbali unavyovifahamu katika mazingira yako. Unapojaribu kuhusianisha kile unachokisoma na maisha yako ya kila siku, unaurahisishia ubongo wako kazi ya kupokea kuliko kuingiza kitu kipya kisichohusiana kwa vyovyote vile na ...
DUH! UMEBADILISHA KICHWA CHA HABARI?
JibuFutaAU.......
La kuvunda halina ubani!
JibuFutaUtalipatia ubani gani la kuvunda? Llikishavunda harufu yake ndo marashi yake tena.
Koero, sijabadili. Pengine ni kwa sababu nimepost zote na hiyo ya juu kwa muda unaokaribiana!
JibuFutaSubi, labda tuliweke kwenye jokofu, waonaje?
La kuvunda halina ubani, kifo hakina kinga,
JibuFutala kuvunda! Hata ukiliweka kwenye jokofu , litavunda tu, la kuvunda, hata kama sio leo, wala kesho, hata mtondo go, iko siku litavunda tu, kuliweka jokofuni, waliongezea tu siku za kutovunda! lakini litavunda tu.
La Kuvunda halina ubani
JibuFuta