Habari za siku ndugu msomaji. Binafsi sijambo. Nafurahi kurejea kibarazani baada ya heka heka za huko na huko. Itoshe kuhusu mimi, nikukaribishe tena humu ndani. Leo ningependa kukusimulia kisa kimoja. Nikuase kwanza, kwamba usilazimike kunielewa vibaya. Sijawa na tabia ya kuona makosa zaidi niwapo mahali ama nikutanapo na watu. Maana siamini kwamba binadamu ana kazi ya kushabikia makosa kuliko jema moja. Nisijitetee sana. Jumapili hii nilipata fursa ya kuhudhuria ibada kwenye kanisa la 'kisomi'. Washirika wa kanisa hili, wengi wao ni wale ambao umande haukuwazuia kuhudhuria shule. Wamesoma. Pamoja na ukweli kwamba wote walikuwa weusi kama mimi, lakini ilikuwa bayana kwamba kiingereza kilikuwa 'nguzo' ya ibada hiyo. Hilo halikuwa tatizo kwangu. Maana inaeleweka kwa wengi wetu kwamba, kusoma kunathibitishwa na umahiri wa kusema kiingereza. Nshazoea hili. Pamoja na ukweli kwamba kiuhalisia kiswahili ndicho kinachotawala madarasani lakini watu hatutaki kuukubali ukweli...
DUH! UMEBADILISHA KICHWA CHA HABARI?
JibuFutaAU.......
La kuvunda halina ubani!
JibuFutaUtalipatia ubani gani la kuvunda? Llikishavunda harufu yake ndo marashi yake tena.
Koero, sijabadili. Pengine ni kwa sababu nimepost zote na hiyo ya juu kwa muda unaokaribiana!
JibuFutaSubi, labda tuliweke kwenye jokofu, waonaje?
La kuvunda halina ubani, kifo hakina kinga,
JibuFutala kuvunda! Hata ukiliweka kwenye jokofu , litavunda tu, la kuvunda, hata kama sio leo, wala kesho, hata mtondo go, iko siku litavunda tu, kuliweka jokofuni, waliongezea tu siku za kutovunda! lakini litavunda tu.
La Kuvunda halina ubani
JibuFuta