Yapo mambo mengi katika jamii zetu yaliyofanyika zamani ambayo tukiyatazama twaweza kujifunza mengi. Mengi ya hayo, si sehemu ya jamii za kisasa hivi leo, lakini yalekuwa na msaada wa namna Fulani kwa jamii. Katika jamii ya asili ya wanyaturu, kabila dogo linalopatika katika wilaya ya Singida (na kidogo manyoni), mahusiano kati ya baba na mama yalikuwa na sura tofauti sana na ilivyo leo. Wakati leo hii, wazazi kulala vyumba tofauti huchukuliwa kama ishara ya kufifia kwa mahusiano baina ya wawili hao, kwa Wanyaturu hiyo ilikuwa na maana tofauti. Kikawaida, wazazi wa Kinyaturu hawakupaswa kukaa nyumba moja (sio chumba kimoja, nyumba moja) ndani ya boma. Katika boma analojenga mwanaume kama himaya ya familia yake, alipaswa kuzingatia uwepo wa nyumba mbili ndnai ya boma moja. Baba ambaye ndiye mkuu wa boma, alilala na wanawe wa kiume katika sehemu maalumu ya nyumba inayojulikana kama "Idemu/Ikumbu". Nyumba hiyo ilijitenga pembeni na nyumba kuu alikoishi mama na wanawe wa...
kaka Bwaya, hapa kazi hipo.Darasa kali, kazi kwelikweli
JibuFutaUkweli ndiyo huo,jamii imetufundisha kuukubali uongo ili tujisikie nafuu.
JibuFutaKaka bwaya kuna kitu ninajiuliza ni kwanini tulipokuwa wadogo tuliambiwa kumpa mtu kitu kwa mkono wa kushoto ni kukosa adabu?Wanablog naomba msaada wenu?
Kweli kabisa,Ndg Bwaya.Ndio maana baadhi ya watawala wanachotaraji katika hotuba zao ni makofi,vigeregere,shwangwe,vifijo,nderemo,makofi,nk...akizomewa,basi hapo hapakaliki.
JibuFutaTatizo kubwa ni kwamba tukiambiwa ukweli huwa tunakasirika na kuwa wakali, lakini pamoja na hayo mi bado napenda kuambiwa ukweli ila tu uwe kwenye soft language kidogo
JibuFutaYule bwana aliyewahi kusema kuwa dunia hii ina umbo la bapa kama meza alionekana mkweli, lakini yule aliyesema kuwa dunia ina umbo la duara aliswekwa lupango kwa na mfalme kwa kusema uongo.
JibuFutakaka Bwaya leo hii ukisema kuwa njia hii ya kuchagua viongozi wetu kwa kutumia nadharia ya Wagiriki wenyewe wanaita Demokrasia haitufai bali turejee kwenye zile njia zetu za asili za kuwapata viongozi walizotumia mababu zetu utaonekana mwehu na juha.
Habari za hapa Kaka Bwaya.
JibuFutaNimepita hapa kibarazani kwako kujitambulisha kuwa nimefungua kijibaraza changu kitakachokuwa kikijihusisha zaidi na masuala ya vijana.
Nimekuwa nimsomaji wa blog yako kwa muda mrefu, na sasa nimeamua na mimi nijitose uwanjani ili kuongeza mchango katika kuielimisha jamii.
Niko ntayari kuelimishwa na kukosolewa pale nitakapoonekana natoka nje ya mstari.
Natarajia ushirikiano wako.
Digna
Bennet na Digna karibuni sana. Nafurahi kuwapokea kama wadau muhimu wa kibaraza hiki.
JibuFuta