Mjadala wa dini na sayansi unaendelea...
Najaribu kupangilia mambo yangu niweze kujadili masuala ya dini wakati wowote kuanzia sasa. Wadau wa masuala haya ninawakaribisha nyote. Jana nilianza kwa kujiuliza swali kuu: Je, ni dini inaiogopa sayansi ama sayansi ndiyo inayoiogopa dini? Mdau wa mjadala huo, Profesa Matondo alikuwa na mchango huu wa kusisimua: ' ''Hili ni suala zito ambalo limehangaisha mafilosofa kwa muda mrefu sana. Kuna mambo ambayo sayansi haijaweza kuyaeleza. Dini kwa upande wake, kwa vile haihitaji vithibitisho kama vile sayansi, inaweza kujibu kila kitu kwa mwenye imani. Kuna mzozo mkubwa sana unaendelea hapa Marekani kuhusu ufundishaji wa nadharia ya Evolution ya Charles Darwin. Walokole wa hapa Marekani wanataka ama ifutiliwe mbali kufundishwa mashuleni au uumbaji (creationism) wa Mungu pia nao ufundishwe kama nadharia mbadala (alternative theory). Wanasayansi wanabisha kwamba uumbaji hauwezi kuthibitishwa kisayansi kama kweli ulitokea na kwa hivyo hauwezi kufundishwa mashuleni. Sij...