Machapisho

Mhe. Zitto ni mwanablogu

Picha
Pamoja na kutumia nyenzo za uandishi wa kiraia kama twitter, facebook na majamvi ya kijamii kama Jamiiforums nk, Mhe. Zitto Kabwe ni mwanablogu. Na blogu yake imesheheni elimu na maarifa ambayo tunayahitaji kwenye majikwaa haya ya kiraia. Ameitambulisha blogu yake siku chache zilizopita (tarehe 25 Mei) kwa maneno machache yafuatayo: "Ndugu msomaji, nimekuwa na blogu hapo kabla lakini sikuweza kuifanyi kazi kama invyostahili. Nimeamua kuanzisha blogu hii mpya ili liwe jukwaa la kujadiliana jinsi ya kuimarisha demokrasia nchini kwetu Tanzania, Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Karibu kwa maoni, ushauri na hata makatazo!" Bonyeza hapa kumsoma , halafu uone namna mwanasiasa huyu kijana alivyotofauti na wanasiasa wazee wasiojua kingine zaidi ya redio na magazeti ya kila wiki. Hawajui kwamba zama hizo zilishapita na hazitarudi tena. Karibu sana Mhe. Zitto.

Ni usalama wa Taifa au ni ubaguzi wa rangi?

Picha
Tuko ndani ya uwanja wa ndege wa Sao Paulo, Brazil. Ni usiku, tunangoja usafiri wa kwenda Dubai, kama lisaa limoja lijalo. Nimekamata kitabu changu nasoma. Ni kitabu cha rafiki yangu kanigawia nionje yaliyomo. Yeye naye kakaa zake kimya anasoma kitabu changu pia. Saa nyingine tunafunika vitabu, tunazungumza mawili matatu, tunaendelea kupekua pekua. Ni katika kuongoja tu usafiri. Faizul, Deo, Bijoy, na mimi jijini Sao Paulo. Picha: Dr Awab Mara wanatufuata watu wawili waliovaa kiraia. Mmoja kajazia, kajichora tatuu mkononi, kavaa viatu vinavyompyaya. Mtu wa mazoezi. Mwingine mdogo dogo tu, ila shida yake hasemi kiingereza. Kwa hiyo ni "mpole fulani hivi". Baunsa anatuonesha kitambulisho chake. Ni askari wa Kibrazil. "Ninaomba kuona hati yako ya kusafiria tafadhali?"askari bonge ananiambia, mwenzie akimsaidia kwa macho. Nilisita kidogo, nikijiuliza inakuwaje aje kwangu wakati nilikuwa na wasafiri wengine. Ndicho nilichomwuliza. Baada ya kudai kuwa anafanya ...

Blogu zakutanisha wanablogu...!

Picha
(picha mali ya Mtanga wa Mwananchi mimi) Habari za kukutana kwa wenzetu watano nilizipokea kwa furaha kubwa. Hii kwa hakika ni hatua kubwa na ya kupigiwa mfano. Bila shaka, kama wanavyofikiri wanablogu wengine, huu utakuwa mwanzo mzuri kwa wengine wetu tukukutana mmoja mmoja na hatimaye wote kwa wakati mmoja kama walivyofanya wenzetu hawa. Hongereni sana Mwananchi mimi , Hadubini , Mtambuzi , Lundunyasa na Chacha Wambura kwa kutuonyesha njia. Wapo watu wanadhani matumizi ya majina bandia yanawasaidia. Niliona mjadala fulani kwenye mtandao wa Jamii forums ambao kwa kweli ni vigumu wanachama wake kukutana kama walivyofanya wenzetu. Bonyeza hapa uone na utafakari. Tuachane na hao wasitaka kufahamika. Turudi kwa wenzetu waliweza kuutumia mtandao mpaka wakaweza kukutana siku ile. Hivi ndivyo Ndugu Fadhy anavyosimulia tukio hili: "Muda huu hapa hoteli ya Movenpick jijini Dar es Salaam. Tunamshukuru sana Mungu kwani leo tumeweza kukutana tena bloggers kama unavyotuona...

Ya Santiago na nguvu za Kiraia

Mkutano uliokusanya wanablogu, wanahabari, wanaharakati na wanateknolojia watokao katika nchi mbalimbali umemalizika. Siku mbili za mwanzo zilihudhuriwa na watu wa kada mbalimbali kutoka hapa Chile na sehemu nyinginezo ikiwa ni pamoja na Kampuni za google, Yahoo, You tube na wengineo. Kilichokuwa muhimu sana katika siku hizo mbili za mwanzo, ni kutizama mifano ya namna uandishi wa kiraia (mablogu, twita, facebook, simu nk) ulivyoweza kushika kasi katika nchi mbalimbali zinazoendelea. Unaweza kusoma muhtasari hapa kuona namna blogu zinavyoleta mageuzi nchini Madagaska kupitia jumuiya ya wanablogu iitwayo Foko . Nilizungumza na Lova Rakotomalala juzi na nilishangazwa na jinsi jamaa wanavyoweza kufanya mambo makubwa katika mazingira magumu yanayofanana na yetu. Madagaska wamekuwa mfano mzuri wa nguvu ya uandishi wa kiraia. Siku zile mbili za mkutano zilitupa ushahidi wa wazi wazi wa namna uandishi wa kiraia unavyopamba moto katika nchi zinazoendelea. Bofya hapa uone mifano mic...

Mkutano wa wanablogu Santiago

Picha
Nimepata fursa ya kukuhudhuria mkutano wa wanablogu wa jumuiya ya Global Voices unaofanyika kwenye Ukumbi wa Maktaba ya Taifa, Santiago Chile. Moja ya vivutio vya mkutano huo ni kukutana na mwanablogu wa kitanzania aishiye Australia Bw. Joe Nambiza Tungaraza na Njeri Wangari mwanablogu wa mashairi wa Kenya .

Ubabe wa dini wa kuhodhi maarifa isiyonayo

Dini kama msamiati, inaeleweka. Lakini tafsiri rasmi naweza kusema ni vigumu kuipata maana inategemeana mara nyingi na matakwa, maoni, makusudi ya huyo anayetafuta maana. Wapo wanaotafsiri dini kwa kuhusisha na dhana ya Mungu kama msingi mkuu wa dini. Wengine wanatafsiri dini kwa kuihusisha na masuala ya ‘kiroho’ yaani spirituality, hisia na imani. Wengine wanaposikia dini mawazo yao yanakimbilia kwenye ‘vyama vya ushabiki wa kiroho’ yaani makanisa, misikiti, mahekalu na vitu kama hivyo. Inachekesha kwamba neno tunalolitumia mara zote, eti linatusumbua kulitafsiri. Sababu ni kwamba tafsiri sahihi yapaswa kuwa ile itakayotuwezesha kuzikusanya ‘dini’ mbalimbali kwa pamoja. Mkusanyiko huu hauwezi kufanywa kwa matumizi ya tafsiri ya dini fulani tu. Kwa maana hiyo, tunaweza kuzikusanya dini zote kwa kusema kwamba ni jumla ya imani zinazohusiana na vile tusivyoviona kwa macho, zinazojaribu kuleta majibu juu ya mikanganyiko ya maisha ili kuleta namna fulani ya matumaini ama ridhiko la ...

Mjadala wa dini na sayansi unaendelea...

Najaribu kupangilia mambo yangu niweze kujadili masuala ya dini wakati wowote kuanzia sasa. Wadau wa masuala haya ninawakaribisha nyote. Jana nilianza kwa kujiuliza swali kuu: Je, ni dini inaiogopa sayansi ama sayansi ndiyo inayoiogopa dini? Mdau wa mjadala huo, Profesa Matondo alikuwa na mchango huu wa kusisimua: ' ''Hili ni suala zito ambalo limehangaisha mafilosofa kwa muda mrefu sana. Kuna mambo ambayo sayansi haijaweza kuyaeleza. Dini kwa upande wake, kwa vile haihitaji vithibitisho kama vile sayansi, inaweza kujibu kila kitu kwa mwenye imani. Kuna mzozo mkubwa sana unaendelea hapa Marekani kuhusu ufundishaji wa nadharia ya Evolution ya Charles Darwin. Walokole wa hapa Marekani wanataka ama ifutiliwe mbali kufundishwa mashuleni au uumbaji (creationism) wa Mungu pia nao ufundishwe kama nadharia mbadala (alternative theory). Wanasayansi wanabisha kwamba uumbaji hauwezi kuthibitishwa kisayansi kama kweli ulitokea na kwa hivyo hauwezi kufundishwa mashuleni. Sij...

Dini inaiogopa sayansi?

Nilitegemea kwamba dini na sayansi vingeenda pamoja. Kwa sababu nionavyo mimi, upo uhusiano mkubwa kati ya vitu hivyo viwili. Kwanza, vyote vinahusu maisha ya watu japo kwa namna tofauti. Lakini pili si lazima viwili hivyo vitengane ili kujenga heshima yake. Lakini ajabu, karibu mara zote tangu maendeleo ya sayansi maumbile yanaanza inaonekana wazi kuwa dini imekuwa kinyume nayo. Je, ni hali hii ni halisi au ni hisia? Je, ni dini inaiogopa sayansi ama sayansi ndiyo inayoiogopa dini? Nitafafanua nikirudi

Blogu mpya nyingine

Picha
Sogea karibu usome blogu ya Ndugu Renatus Kiluvia . Yeye ni mwandishi wa habari na mtangazaji wa kituo cha redio cha 87.8 Ebony fm cha Iringa lakini kwa sasa yuko kwenye studio ndogo ya Dar. Kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe, blog hiyo inahusu muziki na maisha katika nyanja tofauti-tofauti. Pia itahusika kuzungumzia burudani zingine kama filamu n.k. Bonyeza hapa upate kila kitu .

Stella mwanablogu mpya

Kila siku jamii ya wanablogu wa kiswahili inazidi kupanuka. Hivi sasa zipo blogu za kiswahili zaidi ya mia mbili na zinaendelea kuongezeka. Dada yetu Stella naye kajiunga na jamii yatu. Bofya hapa kumkaribisha , kuona maudhui ya blogu yake na pia kuendelea kumsoma. Dada stella, karibu sana.

Kutoka Maktaba: Ndesanjo unaombwa kurudi kundini

Picha
Katika safari ya kupitia kilichomo kwenye maktaba yetu, niliyoisemea kidogo jana, nilimfuma mdogo wangu anayenifuata, akirejea makala za mwandishi Ndesanjo Macha. Makala hizi ni zile alizoziandika kati ya mwaka 2005 mpaka 2007 katika magazeti ya Mwananchi Jumapili. Wakati huo mdogo wangu akiwa kidato cha tano na sita alianza kuzifuatilia kama matokeo ya mkumbo tu (pengine) lakini baadae ukawa ndio ugonjwa wake mpaka zilipotoweka ghafla zaidi ya miaka miwili iliyopita. Sasa akiwa anamaliza Chuo Kikuu mwaka 2010, makala hizo anazisoma kwa kupitia 'hifadhi' ya magazeti yale ya chumbani kwetu. Nimeshawahi kumkuta mwaka jana akiwa na vipisi vya safu ya "Rai ya Jenerali" vyenye tarehe za mwaka 1995 mpaka 2005 vikiwa vimeungamanishwa kwa pamoja na kufanya kitu kama kitabu fulani hivi ambacho alikuwa akitembea nacho kwenye begi lake. Kwa hiyo sikushangaa kukutana na shughuli hii ya kukusanya makala za Ndesanjo hivi majuzi. Picha hizi ni ombi maalumu kwa Ndesanjo M...

Amana ya ‘nguvu zangu’

Picha
Hivi majuzi, nilipata fursa ya kula pasaka nyumbani kwetu, Singida. Katika niliyoyafanya, ni pamoja na kukagua ‘maktaba’ ambayo mzee wangu alitutengenezea chumbani kwetu. Ni kijishelfu kidogo ambacho alikitumia enzi hizo kutuwekea vitabu kadhaa kila mara na kutuhimiza kuvisoma. Pamoja na vitabu, humo aliweka nakala za magazeti ya Rai ile ya zamani na mengineyo. Na kweli tuliyasoma, mimi na mdogo wangu. Namshukuru baba yangu kwa hilo. Maana nakumbuka alinifanya nianze kugharamia nakala za magazeti tangu nikiwa kijana wa darasa la sita na saba. Niliweza kubana matumizi ili kumudu kununua gazeti hilo kila wiki. Ndio ulikuwa ulevi wangu. Pia nimshukuru kwa sababu alinijengea ari ya kuiba vitabu kila nilikopita. Ujue kila mtu hukumbuka siku zile za ‘adolesensi’ kwa jinsi yake. Wengine kwa idadi ya wasichana aliowatongoza. Wengine kwa michezo ya ‘baba na mama’. Na kadhalika. Mimi huzikumbuka zaidi kwa wizi wa vitabu. Sikuwa na uwezo wa kumudu kununua vitabu nilivyovipenda. Kwa hiyo ...

Arusha warembo ni majasiri wa kibiashara

Picha
Nimewapenda akina dada hawa wanaojishughulisha na biashara halali kama hizi. Ni majasiri wasiosita kufanya shughuli kama hizi kujipatia kipato licha ya urembo wao. Hapa niliwafuma wakimsubiri mwenzao. Then wakaendelea na shughuli zao. Pongezi kwao.

Padre Karugendo ndani ya Blogu

Kama ulizoea kusubiri siku ya Jumatano kusoma mawazo ya Padre Karugendo kwenye gazeti la Raia mwema au labda Jumapili kwenye Tanzania Daima, jua enzi hizo zimepita. Sasa utaweza kupata kila unachotaka kwa wakati wowote kupitia blogu yake. Bonyeza hapa kumkaribisha , halafu uendelee kumtembelea. Karibu sana Padre Karugendo. Umechagua fungu jema kufungua blogu.

Tangazo la Mkutano Mkuu wa Uanahabari wa Kiraia wa Global Voices 2010

Picha
Mkutano wa wanablogu wa Global Voices, utafanyika Mjini Santiago mwezi Mei tarehe 6 na 7 mwaka huu. Nimezipata habari hizo kupitia ukurasa wa kiswahili wa mradi wa Lingua Swahili . Nimetamani kama na sisi tungekuwa tunapanga kukutana siku fulani mwaka huu! Inawezekana! Ni muhimu tuanze kufikiri kukutana uso kwa uso hata kama matanga ya ile Jumuiya yetu hajapita bado.