Heri ya mwezi mpya!
Mwezi wa tano ndio huu. Tarehe mbili leo. Kama ulikuwa hujapanga cha kufanya mwezi huu, ndugu, hujachelewa. ( Si unajua haipendezi kufanya chochote bila kupanga?) Tabia ya kusubiri mwisho wa mwaka ndio tuanze kufikiri kupanga mipango mingi ya mwaka mzima ( ambayo hata hivyo haitekelezeki) si nzuri sana. Nakukumbusha mipango yako ya mwaka huu: Ulipanga kufanya nini mwaka huu? Je, umefikia walau nusu ya mipango yako? Una mikakati gani na mwezi huu wa tano? Nusu ya mwaka ndo inayoyoma! Nakukumbusha kutafakari upya mambo yako mwaka huu, uone wapi umefanikiwa na wapi unahitaji kujipanga vyema zaidi. Nakukumbusha kutafakari changamoto ulizokumbana nazo katika sehemu ya kwanza ya mwaka huu, na ufikiri namna ya kukabiliana nazo vizuri zaidi kwa nusu iliyobaki. Na unapofanya hivyo, usiache kupitia hapa kuanzia juma hili kwa ajili ya vipande vya saikolojia na falsafa za kutafakari pamoja namna ya kujielewa. Niwatakieni wanablogu wote heri ya mwezi mpya wenye mafanikio (pamoja na uki...

Ntakitafuta hicho Mkuu!
JibuFutaIla MKUU una ukimya fulani siku hizi MKUU!
Just sayin'.....!
Ni kweli mtakatifu Kitururu. Kuna mambo hayajakaa sawa bado.
JibuFutaElimu ya watanzania iliwafanya wananchi wachukie vitabu sababu toka shule za misingi hadi vyuo vikuu vitabu vinaelezea matukio ya ukoloni, historia zisizokuwa na mizizi ya mtu kuwa mbunifu na mfumo mbovu wa hatima ya elimu kuwa mwenye akili ni yule anayefaulu mtihani wa mwisho.
JibuFutaChachu ya kusoma vitabu ijengwe kutoka mashuleni, watu wanaona bora atembee mtaani kuuza mitumba ya CD/DVD apate riziki kuliko kusoma vitabu mwisho wa siku alale njaa.
NAKUKARIBISHA HUKU PIA, http://www.amosmsengi.blogspot.com/
Kaka habari za siku, naona hata namba zako za simu hasa TIGO haipatikani........
JibuFutaKuhusu kitabu, ni kweli kinaonekana ni kizuri, lakini naomba wakati mwingine uwe unatuelekeza vinapopatikana vitabu hivyo..... ni wazo tu mkuu
Pamoja daima
Amos asante sana kwa maoni yako murua. Karibu kwenye uwanja wa kublogu.
JibuFutaKoero, asante kwa wazo zuri.