Kama sio utumwa ni nini hiki?
Habari za siku ndugu msomaji. Binafsi sijambo. Nafurahi kurejea kibarazani baada ya heka heka za huko na huko. Itoshe kuhusu mimi, nikukaribishe tena humu ndani. Leo ningependa kukusimulia kisa kimoja. Nikuase kwanza, kwamba usilazimike kunielewa vibaya. Sijawa na tabia ya kuona makosa zaidi niwapo mahali ama nikutanapo na watu. Maana siamini kwamba binadamu ana kazi ya kushabikia makosa kuliko jema moja. Nisijitetee sana. Jumapili hii nilipata fursa ya kuhudhuria ibada kwenye kanisa la 'kisomi'. Washirika wa kanisa hili, wengi wao ni wale ambao umande haukuwazuia kuhudhuria shule. Wamesoma. Pamoja na ukweli kwamba wote walikuwa weusi kama mimi, lakini ilikuwa bayana kwamba kiingereza kilikuwa 'nguzo' ya ibada hiyo. Hilo halikuwa tatizo kwangu. Maana inaeleweka kwa wengi wetu kwamba, kusoma kunathibitishwa na umahiri wa kusema kiingereza. Nshazoea hili. Pamoja na ukweli kwamba kiuhalisia kiswahili ndicho kinachotawala madarasani lakini watu hatutaki kuukubali ukweli...

Ntakitafuta hicho Mkuu!
JibuFutaIla MKUU una ukimya fulani siku hizi MKUU!
Just sayin'.....!
Ni kweli mtakatifu Kitururu. Kuna mambo hayajakaa sawa bado.
JibuFutaElimu ya watanzania iliwafanya wananchi wachukie vitabu sababu toka shule za misingi hadi vyuo vikuu vitabu vinaelezea matukio ya ukoloni, historia zisizokuwa na mizizi ya mtu kuwa mbunifu na mfumo mbovu wa hatima ya elimu kuwa mwenye akili ni yule anayefaulu mtihani wa mwisho.
JibuFutaChachu ya kusoma vitabu ijengwe kutoka mashuleni, watu wanaona bora atembee mtaani kuuza mitumba ya CD/DVD apate riziki kuliko kusoma vitabu mwisho wa siku alale njaa.
NAKUKARIBISHA HUKU PIA, http://www.amosmsengi.blogspot.com/
Kaka habari za siku, naona hata namba zako za simu hasa TIGO haipatikani........
JibuFutaKuhusu kitabu, ni kweli kinaonekana ni kizuri, lakini naomba wakati mwingine uwe unatuelekeza vinapopatikana vitabu hivyo..... ni wazo tu mkuu
Pamoja daima
Amos asante sana kwa maoni yako murua. Karibu kwenye uwanja wa kublogu.
JibuFutaKoero, asante kwa wazo zuri.