Machapisho

Madhara ya Kutoa Ushauri Kienyeji na Kuugeuza Unasihi kuwa Ushauri

Picha
Utamaduni wa (kutoa na kuomba) ushauri umejengeka kwenye misingi ya hekima ya wazee walioona mengi, uzoefu wa mtu mzima unaompa uhalali wa kutoa mwongozo wa kufuata kwa anayemzidi.  Hata tunaposikia unasihi (counselling), aghalabu, mawazo yetu yanaenda kwenye taaluma ya kushauri watu na kuwaambia cha kufanya ili kutatua matatizo yanayowakabili. Wapo, tena wengi, wanaotafsiri ‘counselling’ kama ushauri. Counselling sio ushauri. Katika makala haya, ninajenga hoja kuwa kutoa ushauri ni jambo la hatari na kwamba linaweza kusababisha madhara makubwa kwa anayeshauriwa lakini pia hata anayeshauri.  Kadhalika, ninalenga kuonesha, japo kwa ufupi kuwa hata kwenye unasihi msingi wa kwanza wa kuzingatia kwa mtoa huduma (aliyefuzu) ni kuepuka kabisa kutoa ushauri kwa mtu. Nakusudia kuonesha nini hasa huwa ni malengo ya unasihi. stefanamer/Getty Images Ushauri ni nini?  Unaposema unamshauri mtu unakuwa na maana gani?  Ushauri, kwa kifupi, ni maelekezo mahususi unayompa mtu, maamuz...

Changamoto za kuwanyima watoto kufurahia utoto wao

Picha
  Tunaishi kwenye dunia inayopitia mabadiliko mengi. Mabadiliko haya ya kijamii na kiuchumi, kwa kiasi kikubwa, yamezidisha matarajio tuliyonayo kwa maisha. Ukiacha matarajio mengi tuliyonayo kwetu binafsi, kuna matarajio mengi hata kwa wenzi wetu. Mke, kwa mfano, anatarajia mume awe kila kitu anachokifahamu kuhusu mwanamume. Mume ana kazi ya kuwa mcha Mungu, mtu wa sala, mtafutaji na mchapa kazi hodari, mcheshi, rafiki msikivu, kiongozi bora,     baba mzuri na mume mzuri asiyechelewa kurudi nyumbani. Matarajio haya makubwa yana faida zake lakini pia yana upande wa pili unaochanga migogoro mingi katika familia.   PICHA:  Wikimedia Commons   Hatuishii kuwa na matarajio makubwa kwa wenza wetu. Tunazidisha pia matarajio kwa watoto wetu kiasi cha kuwanyima fursa ya kufurahia utoto wao. Hebu fikiria mtoto asiyeruhusiwa kufanya makosa. Kila analojaribu kufanya, anapodadisi mazingira yake,  anakuwa anatafsirika kama mtoto asiye na nidhamu na adabu kwa wa...

Ukishasahau ulikotoka huwezi kuwa mzazi mzuri

Picha
  Sijui kama umewahi kuwaza kama mimi. Je, mafanikio yetu yanawasaidia watoto kuwa binadamu timamu? Je, uwezo tulionao kiuchumi unawezesha watoto kujifunza tabia zitakazowafanikisha kiuchumi? Kuna namna ninaogopa kuwa huenda tunawanyima watoto wetu fursa ya kujifunza maisha katika uhalisia wake. Nafahamu wapo baadhi ya wazazi wamekulia kwenye familia zinazojiweza kiuchumi. Hata hivyo, hiyo haiondoi ukweli kuwa wengi wetu tumetoka kwenye familia masikini na tumekuwa kizazi cha kwanza kupambana na kuuweza umasikini. Je, tunawaandaa watoto wetu kujikwamua kama tulivyojikwamua sisi?   PICHA: Marlous de Milliano Tunafahamu namna umasikini unavyofedhehesha. Umasikini unafanya maisha yako yasiwe na uchaguzi. Umasikini unakufanya upate kinachopatikana na sio kile unachokihitaji.  Hili, pamoja na ubaya wake, kwa kiasi kikubwa limekuwa kichocheo cha wengi wetu kuwa na hasira kubwa kupambana na umasikini kwa nguvu zote. Bidii ya kazi unayokuwa nayo ni matokeo ya hasira kuwa usi...

Una nguvu ya kupambana na hali iliyokuchosha

Umewahi kujiuliza kwa nini mtu anapigwa, anaumizwa, anadhalilishwa na mpenzi wake na bado haoni kama kuna kitu anaweza kufanya? Mwingine anasitisha uhusiano lakini anapoanzisha mahusiano anakutana na mwingine mwenye tabia zile zile alizozikimbia kwa aliyemwacha. Ili kulitafakari hili, nikusimulie alichokifanya Martin Seligman na Steven Maier mwaka 1965. Washunuzi hawa waliwatia mbwa kifungoni kwa kuwafungia kwenye kizimba kisichowaruhusu kutoka. Mle ndani kizimbani mbwa walipigwa shoti ya umeme mfululizo iliwapa maumivu makali. Hata pale ambapo mbwa angefanya majaribio ya kutoroka asingeweza. Kizimba kilikuwa imara. Kilichowashangaza Seligman na Maier ni kwamba hata pale walipofungua mlango wa kizimba kuwaruhusu watoke, ingawa mbwa wale walilia kwa uchungu, wakilalamika na kutia huruma, hawakuthubu kujaribu kutoka pamoja na maumivu makali ndani ya kizimba. Hali ilikuwa tofauti kwa kundi jingine la mbwa lililokuwa limefungiwa kwenye kizimba kisicho na shoti ya umeme au kilichokuwa na uw...

Kikao cha tathmini na mipango ya familia

Picha
Wiki hii mimi na familia yangu tulikuwa na kikao cha ‘halmashauri kuu’ ya mwaka. Kikao chenyewe kililenga kujitathmini sisi kama familia na kujiwekea malengo ya pamoja kwa mwaka 2023. Kikao hiki kinatarajiwa kufuatiwa na kikao cha 'Kamati Kuu.' Maandalizi ya kikao hiki cha 'banguabongo' yalifanyika kwa kupeana dondoo za kufanyia kazi agenda za kikao. Hatimaye siku ikawadia. Jioni ya Jumapili ya Desemba 25, 2022. Tukiwa eneo tulivu mbali nyumbani, baada ya mwenyekiti wa kikao kueleza kwa nini tumekutana, shughuli yenyewe ikaanza. Agenda ya kwanza ilisomwa na mtoto wetu wa kwanza, “Kitu gani ulichofanya mwaka huu kinakufanya ujisikie fahari?” Tukatakiwa kuandika kwenye vikaratasi vidogo tulivyokuwa tumegawiwa tayari. “Tumieni vikaratasi vya kijani. Mambo matano makubwa yaliyokufanya ukajisikia fahari kwa mwaka huu.” Baada ya kila mmoja kuorodhesha mambo yake matano yaliyomwendea vyema mwaka huu, mtoto wa pili akakusanya vikaratasi vyenye majibu na kuvibandika kwenye u...

Tutafakari hatari ya ‘malezi ya bweni’

Picha
PICHA:  Aparna Wazazi hawaamui tu kuwapeleka watoto wadogo kusoma shule za msingi za bweni. Ukiwasikiliza, mara nyingi wanakuwa na sababu za msingi kufanya maamuzi hayo magumu. Masuala kama migogoro ya kifamilia, wazazi kutokupatikana nyumbani, kutokuaminika kwa walezi mbadala mfano, wadada wa kazi, ni baadhi ya sababu zinazowafanya wazazi waamue kulipa gharama kubwa ya kuwakabidhi watoto kwa walezi wanaoaminika shuleni. Nafahamu wapo wazazi wanaochukulia shule za bweni kama sehemu ya kuonesha uwezo wao wa kifedha. Kwa mfano, baadhi ya wazazi hususani wale wenye uwezo wa kifedha, huzifikiri namna nzuri ya kuonesha ‘kujali elimu ya mtoto’ ni kumpeleka kwenye shule ya gharama kubwa na hata ikibidi shule ya msingi ya bweni ‘ili mtoto akazingatie masomo na apate muda wa kutulia.’ Hawa ni wachache lakini wapo. Shule pia zinazowaaminisha wazazi kuwa taaluma inapatikana bweni nazo zipo. Saa nyingine ni mchanganyiko wa nia njema, biashara au basi tu kukosa uelewa. Ukweli unabaki kwamb...

Unampeleka mtoto mdogo bweni? Fikiria.

Picha
Miaka michache iliyopita, mtu ulikuwa ukisikia shule za msingi za bweni, tena kwa watoto wadogo, tafsiri unayopata kwa haraka haraka ni malezi mabovu. Unampelekaje mtoto wa miaka sita bweni? Kuna nini cha maana shule ya bweni kinachohalalisha mtoto kutengwa na wazazi wake? Kwa hiyo, tuliona bweni ni uamuzi wa mzazi asiyeelewa jukumu lake la malezi, mzazi asiyejali, anayeamua kumtelekeza mtoto kwa sababu zisizo na msingi. Lakini kwa hizi nyakati tulizonazo, tunapokabiliwa na mabadiliko mengi ya kijamii, saa nyingine tunahitaji kuwa na tahadhari tunapofanya mahitimisho ya haraka kwa namna hiyo. Sikiliza simulizi la Aisha, afisa wa benki, mama wa mtoto anayesoma shule ya msingi la bweni. “Sikuwahi kufikiri ningekuwa mama anayeona bora mtoto aende bweni. Ndugu yangu yamenikuta.” Aisha ana mgogoro mkubwa na mzazi mwenzake. Ugomvi wao, ananiambia, ulifikia ngazi ya uadui. Haikutosha wao kushindwa kuishi pamoja, lakini pia ikawa vigumu kukubaliana nani abaki na mtoto. “Tulivutana sana. Baad...

Malezi yanapokuwa ‘rasha rasha’ tuilaumu teknonojia?

Picha
PICHA: businessday.ng Kama ambavyo imeanza kuwa vigumu wengi wetu kumaliza siku bila usaidizi wa zana za teknolojia, ndivyo malezi nayo yanavyoanza kuchukua uelekeo wa kuhitaji usaidizi wa teknolojia. Saa nyingine mzazi usingependa watoto waangalie katuni muda mrefu. Lakini unafanyaje sasa kama wewe mwenyewe hata unapokuwepo nyumbani huna mengi ya kufanya na watoto? Ombwe, kwa kawaida, huwa ni muhimu lizibwe. Lakini pamoja na kusaidia kujaza ombwe la sisi wazazi kutokuwepo kwenye maisha ya watoto, bado teknolojia inayo mengi yenye manufaa. Kubwa zaidi ni kuwachangamsha watoto kiakili.  Nitumie mfano wa mwanangu. Hajakamilisha miaka mitatu. Ukikaa naye anayo mengi ya kukusimulia. Uwezo tu wa kusimulia jambo na likaeleweka katika umri wa miaka miwili sikuuona kwa dada yake waliozidiana karibu muongo mzima. Ingawa bado ni mapema mno kumpeleka darasani, anatambua herufi na tarakimu zote, ana uelewa wa awali wa kuhesabu, anafahamu majina ya rangi nyingi, anawafahamu majina na tabia ...