Utaratibu wa Kufuata Unapoachishwa Kazi



Sheria ya ajira na mahusiano kazini Namba 6 ya mwaka 2004 inaainisha mazingira kadhaa yanayoweza kusababisha mwajiriwa aachishwe kazi na mwajiri. Kwanza, kama mwajiri amefuata masharti ya mkataba yanayohusiana na utaratibu wa kumwachisha kazi. Kufuata masharti ya mkataba kunategemea kama aina ya mkataba. Pale ambapo mkataba ni wa kudumu, mwajiri lazima awe na sababu halali za kuchukua hatua za kusitisha mkataba kwa kufuata utaratibu.

 Lakini pia mwajiri anaweza kumwachisha kazi mfanyakazi kwa sababu ya mwenendo mbaya na utovu wa nidhamu kazini. Makosa yanayoangukia kwenye utovu wa nidhamu ni pamoja na kufanya vitendo vya dharau ya kubwa kwa viongozi wako kazini na utoro. Utoro ni kutokuonekana kazini bila taarifa au kuchelewa kufika kazini kinyume na mkataba wa kazi.

Aidha, vitendo vinavyoonesha ukosefu wa maadili vinaweza kuchangia kukuondoa kazini. Kwa mfano, kufanya udanganyifu mkubwa, kuharibu mali za mwajiri wako kwa makusudi, kuhatarisha usalama wa watu wengine kwa makusudi, uzembe mkubwa kazini na hata kumtukana,  kumdhalilisha au kumshambulia mfanyakazi mwenzako, mteja, msambazaji au mwanafamilia au mtu yeyote anayehusiana na mwajiri.

Vyovyote iwavyo, kuachishwa kazi si jambo jepesi. Mbali na athari za kiuchumi, kupoteza kazi bila hiari yako kunaweza kukuathiri kisaikolojia. Athari hizo zinaweza kuwa kubwa zaidi kama utakuwa na hisia kuwa utaratibu uliotumika kukuondoa kazini haukuwa wa haki. Hisia kuwa hukutendewa haki na ukakosa namna ya kupata haki yako zinaweza kukuumiza zaidi.

Ndio kusema, ni busara kujiridhisha kuwa pamoja na yaliyotokea bado unapata haki zako unazostahili. Makala haya yanaangazia mambo mawili ya kufanya unapopewa taarifa rasmi za kusitishwa kwa ajira yako.

Kufuatwa kwa utaratibu

Pamoja na utaratibu wa uachishwaji kazi ulioainishwa kisheria, inawezekana mwajiri kwa kujiona anaweza kufanya lolote, akaamua kukuachisha kwa sababu zake binafsi. Mfano, pengine mwajiri amesikia umeathirika na VVU/UKIMWI na kuamua kukufuta kazi kwa visingizio vingine. Lakini pia inaweza kutokea pamoja na kuachishwa kazi kwa makosa ambayo wewe mwenyewe unajua ni ya kweli, taratibu za kufanya hivyo hazikufuatwa.

Kwa hivyo, hatua ya kwanza baada ya kupewa taarifa rasmi kuwa umeachishwa kazi, ni kujiridhisha kuwa ni kweli utaratibu halali wa kisheria umefuatwa katika kukuachisha kazi. Hapa kuna mambo mawili. Kwanza, mwajiri analazimika kuthibitisha kuwa kuna kosa limefanyika na lina uzito wa kutosha kuhalalisha kuachisha kazi.

Jambo la msingi ni kwamba hata kama umefanya kosa, mwajiri analazimika, kwa mujibu wa sheria, kufanya juhudi za kurekebisha nidhamu yako kwa unasihi (ushauri) na maonyo. Kuonywa kunalenga kukusaidia kuelewa kuwa unapofanya kosa kama hilo unaweza kuchukuliwa hatua zaidi za kinidhamu. Ikumbukwe kuwa mwajiri analazimka kuwafahamisha wafanyakazi sera za nidhamu katika eneo lake la kazi.

Kwa mujibu wa Sheria hii, mfanyakazi anapofanya kosa na mwajiri akaona kuna haja ya shauri kufanyika, basi mwajiri analazimika kumpatia hati ya mashtaka mfanyakazi husika iliyoandikwa katika lugha ambayo mfanyakazi ataielewa. Kisha mfanyakazi atapewa muda wa kutosha (si chini ya masaa 24) kuandaa utetezi. Katika kutekeleza haki hii ya kusikilizwa, mfanyakazi anaweza kujitetea kwa msaada wa vyama vya wafanyakazi au mfanyakazi mwenzake.

Shauri hili litaendeshwa na wakili ambaye atakuwa hakushiriki kwenye mazingira yaliyosababisha kesi. Mfanyakazi atakuwa na haki ya kujibu tuhuma na kuhoji mashahidi watakaoitwa na mwajiri. Hata hivyo, mfanyakazi asipokuwepo bila sababu, shauri lake litaendelea bila yeye kuwepo. Uamuzi ukishafanyika, ikiwa ni pamoja na kuachishwa kazi, mfanyakazi atajulishwa kwa maandishi na kuelezwa sababu za kuachishwa kazi.

Katika mazingira ya kuachishwa kutokana na utendaji mbovu, utaratibu kama huo utachuliwa isipokuwa hapa mwajiri atahitajika kumwezesha mfanyakazi kujifunza kazi kabla ya kuchukua hatua zozote. Kadhalika, pale ambapo mfanyakazi ameachishwa kazi kutoka na ugonjwa au ameonekana hawezi tena kudumu kazi zake shauri ya ugonjwa, mwajiri atahitaji kuongozwa na maoni ya daktari.

Haki unazostahili

Mfanyakazi aliyeachishwa kazi ana haki ya kulipwa kiinua mgongo cha mshahara wa siku 7 kwa kila mwaka kamili wa kuwa katika ajira mfululizo kwa mwajiri huyo kwa miaka isiyozidi 10. Mshahara wa siku unaweza kukokotolewa kwa kugawanya mshahara wa mwezi kwa kila siku.

Hata hivyo ikiwa mfanyakazi aliachishwa kabla ya kuisha mwaka wa kwanza wa ajira, aliachishwa kihalali kwa sababu ya mwenendo mbaya, kukosa uwezo, kutokuhitajika au amekataa kazi mbadala aliyopangiwa basi hatastahili malipo ya kiinua mgongo.

Pia, akiba ya mfanyakazi kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii haitaguswa na mwajiri kwa sababu zozote. Katika mazingira ambayo mfanyakazi ameachishwa kazi akiwa na mkopo benki, itategemea na makubaliano yaliyofikiwa kati yake na benki. Kwa mfano, ikiwa mwajiri ndiye mdhamini wa mfanyakazi benki, kwa maana ya mfanyakazi kutumia mshahara wake kama dhamana, ni jukumu la mwajiri kuwasiliana na benki kuhusiana na deni litakaloachwa.

Haki nyingine unazostahili ni cheti cha utendaji kazi chini ya mwajiriwa anayekufuta kazi, posho ya usafiri kwenda mahali ulikotoka kwa mujibu wa mkataba na mwajiri.

Usuluhishi

Katika mazingira ambayo unaamini hujatendewa haki kwa maana kutokuridhishwa na utaratibu uliotumika kukufuta kazi, una nafasi ya kupata msaada kwenye tume ya usuluhishi wa migogoro ya kazi. Maamuzi ya tume hiyo yataongozwa na kanuni za taasisi za kazi za mwaka 2007 zinazolenga kulinda maslahi ya pande zote.

Hata hivyo, wakati ukishughulikia mgogoro huo kisheria, hupaswi kulazimisha kuendelea na kazi hata kama unaamini ulionewa.

Makala haya yameandaliwa kwa msaada mkubwa wa Janeth Urio, Mhadhiri wa Sheria, Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge (MWECAU) na Wakili wa Mahakama Kuu. Unaweza kumpata kwa simu: 0786-836 220. 

Maoni

  1. Ikiwa nimefanya kazi ndani ya miezi mitatu, na nimesaini mkataba wa mwaka, ila kwenye mkataba kuna kipengele cha majaribio ya miezi mitatu. Je, mwajiri akinisimamisha kazi, haki zangu zikoje kwenye malipo?

    Naomba jibu please. Asante.

    JibuFuta
  2. Ikiwa nimefanya kazi miaka mitatu na sina mkataba wowote,,je ni haki kisheria?

    JibuFuta
  3. Je ni harali kufanyishwa kazi au kuajiliwa Na kampini zaidi ya miaka miwili bila mkataba?

    JibuFuta
  4. Je nikiwa nimefanyisha kazi na raiya wakigeni zaidi ya miaka mili sina mkataba nna kiinuwa mgongo apo kaniachisha kazi kwakunishuku kwamba nimemuibia police ikasibitsha sikafanya wizi huo

    JibuFuta
  5. Napenda kuuliza kwamba he unapokua umepunguzwa kazi ukapewa notice ya yakupungwa Nazi na malipo ya kinua mgongo yatakiwa kutolewa ndani ya Siku ngapi

    JibuFuta
  6. Je unapofanyishwa kazi na kampuni baada ya miaka miwili haijakupatia mkataba.na ikakupatia mkataba baada ya hapo ikakufukuza kazi.swali langu ni kuhusu mafao unatakiwa kupata kuanzia pale mkataba wako unapoanzia au ni kuanzia pale ulipoanzia kazi pamoja na kwamba walichelewa kukupatia mkataba wao? Naomba majibu 0766367032.

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Zilisomwa zaidi wiki hii...

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke-1

Maana ya Saikolojia na Nafasi Yake Katika Jamii -1

Haiba ni nini?

Uislamu ulianza lini?

Pay $900? I quit blogging