kwanza nilidhani dhamira,pili nilidhani ubinadamu,tatu nilidhani nyakati mpya,nne nildhanai ilani ya chama itawekwa kando,tano nilidhani hisia za kweli shauri kaishi mjini.....kumbe ilikuwa kama kawaida wabongo tunavyopenda kusikia neno 'ahadi'. asante kwa kutembelea blogu yangu pia
Global Voices Citizen Media Summit in Cebu, The Philippines in 2015. Photo Courtesy of Global Voices I started my blog in 2005. I was among very few Tanzanians who were inspired by Ndesanjo Macha to start blogging. For those of you who do not know, the history of Tanzanian blogosphere recognizes the contribution of this great man. His influential weekly column in a local newspaper invited many of us to his blog. In fact he was the first Tanzanian to blog in Kiswahili . That was in 2004. I had the privilege of meeting him in Nairobi, Kenya in 2012 and in Cebu, The Philippines in 2015. We were both attending Global Voices Citizen Media Summits. For me, blogging was fun. I never thought that blogs could actually threaten politicians. That was until 2010 when I had an opportunity to attend the Global Voices Citizen Media Summit in Santiago de Chile. I was shocked to hear friends talking about restriction of fr...
Habari za siku ndugu msomaji. Binafsi sijambo. Nafurahi kurejea kibarazani baada ya heka heka za huko na huko. Itoshe kuhusu mimi, nikukaribishe tena humu ndani. Leo ningependa kukusimulia kisa kimoja. Nikuase kwanza, kwamba usilazimike kunielewa vibaya. Sijawa na tabia ya kuona makosa zaidi niwapo mahali ama nikutanapo na watu. Maana siamini kwamba binadamu ana kazi ya kushabikia makosa kuliko jema moja. Nisijitetee sana. Jumapili hii nilipata fursa ya kuhudhuria ibada kwenye kanisa la 'kisomi'. Washirika wa kanisa hili, wengi wao ni wale ambao umande haukuwazuia kuhudhuria shule. Wamesoma. Pamoja na ukweli kwamba wote walikuwa weusi kama mimi, lakini ilikuwa bayana kwamba kiingereza kilikuwa 'nguzo' ya ibada hiyo. Hilo halikuwa tatizo kwangu. Maana inaeleweka kwa wengi wetu kwamba, kusoma kunathibitishwa na umahiri wa kusema kiingereza. Nshazoea hili. Pamoja na ukweli kwamba kiuhalisia kiswahili ndicho kinachotawala madarasani lakini watu hatutaki kuukubali ukweli...
YAMEKUWEPO madai kwamba Uislam ulianza tangu kuumbwa kwa dunia. Na wapo watu wanaotuaminisha hayo. Ukweli ni kwamba Uislam ulianzishwa na Nabii Muhammad mwaka 622 BK huko Arabia. Kabla yake, dini zilizokuwepo zilikuwa ni Uyuda ambayo ni dini rasmi ya Wayahudi (Judaism) na Ukristo ambayo ni dini ya mataifa wasio Wayahudi ulioanza miaka kadhaa baada ya Yesu kuwa ameondoka mwaka 33BK. Yesu mwenyewe hakuanzisha Ukristo. Alisali katika misikiti ya Wayahudi. Masinagogi. Maelezo haya yana msingi wa kistoria na sio propaganda za kidini. Ndio ni propaganda kwa sababu dini zote zimekuwa na tabia ya kuonyesha kwamba zenyewe ndizo za kweli kuliko dini nyinginezo hata ikibidi kwa kuichezea historia. Na ni bahati mbaya kwamba Dini zimekuwa na tabia ya kufanana ya kuzima uwezo wa waumini wake kuhoji lolote kwa kuwajengea hofu ya kujitafutia laana. Qur’an inatupa maelezo yanayokinzana kuhusu lini hasa Uislamu ulianza. Baadhi ya mistari katika kitabu hicho zinadai kwamba ‘nabii’ Muhammad ndiye ...
(picha kutoka Mawazoni bila ruhusa) Ningependa kumwomba mheshimiwa Katibu Mtendaji wa JUMUWATA ruhusa ya kuuliza swali hili. Tumefikia wapi na ile Jumuiya ya Wanablogu Tanzania? Mnaonaje tukifanya mjadala wa wazi kuhusu 'ufufuaji' wa jumuiya yetu? Jamani yasijeyakawa yale ya mwaka elfu tisa mia sabini na saba.
WANAUME wengi wanaamini wanawake, kwa kawaida, ‘wanapenda hela.’ Kwamba ukiweza kumhakikishia mwanamke 'uhakika wa kiuchumi' unakuwa umemaliza. Ingawa hatuwezi kupuuza ukweli kuwa uhakika wa 'kiuchumi' ni moja wapo ya mahitaji ya mwanamke, lakini si sahihi kuamini kuwa moyo wa mwanamke unaweza kuthamanishwa kwa fedha. Fikra hizi walizonazo wanaume [kuwa anachokihitaji mwanamke ni fedha] zimeleta matatizo mengi katika mahusiano na ndoa. Kwa mfano, wapo wanaume ambao baada ya kuhakikisha wenzi wao wamepata mahitaji ya msingi, basi wanawatelekeza kihisia. Hali hii husababisha upweke mkubwa kwa wanawake hawa wanaojikuta hawana mtu wa karibu kuwasikiliza isipokuwa vitu.
Jana nilikuwa nikitazama kipindi cha kiislamu kwenye televisheni ya Chaneli 10. Suala la mali katika ndoa za dini hiyo lilikuwa likijadiliwa. Kwamba Kiislam, mali katika ndoa si suala la wanandoa kwa pamoja. Kwamba mali anazoingia nazo mwanandoa kwenye ndoa, zinabaki kuwa zake mwenyewe. Na wakiachana, kila mmoja anaondoka na alichokuja nacho. Hata ndani ya ndoa, mali zinapatikana 'separately' kwa maana ya kwamba kila anachopata mwanandoa hicho ni haki yake yeye mwenyewe. Wakitengana, kila mtu anaondoka na vyake. Katika kufakari hayo, nilijaribu kumfikiria mwanamke na nafasi yake katika ndoa. Nikamwona kama kiumbe anayenyanyaswa na dini. Kwa nini? Wanaume wengi hutafuta mali kwanza ndio waoe, na hata wanapooa, huwaoa wanawake watakaowategemea wao. Katika hali hii nini salama ya mwanamke katika dini inayoruhusu talaka? Hizi si dalili za wazi za ukandamizaji wa jinsia ya kike?
Mwandishi machachari na mwanafalsafa anayeheshimika kwa uchambuzi makini, Padre Privatus Karugendo (pichani) amevuliwa daraja la Upadre. Habari hizi si njema na ni za kusikitisha sana. Yeye mwenyewe amenukuliwa akisema kuwa hautambui uamuzi huo ambao anaamini umefanyika kwa misingi ya chuki za watawala wa kanisa hilo. Nimeshtushwa na habari hizi kwa sababu kwanza nimekuwa mfuatiliaji wa makala zake kwa maika mingi tangu enzi za Rai ya zamani, na sasa Raia mwema pamoja na Tanzania Daima . Na kwa majuma kadhaa Padre Karugendo amekuwa akiandika mtazamo wake kuhusu namna kanisa la Katoliki (hasa la Afrika) linavyoendeshwa. Yeye anasema watawala wa Kanisa wanatutawala badala ya kutuongoza . Kama na wewe ni msomaji mzuri wa makala zake utakubaliana nami kuwa Padre Karugendo mara zote ameonyesha wazi kuwa Padre anayetaka mabadiliko. Mara zote amejitahidi kuwa yeye zaidi kuliko 'kuigiliza' misimamo asiyoiamini yeye. Si mara moja nimesoma akitofautiana na wakuu wake wa dini kwe...
kwanza nilidhani dhamira,pili nilidhani ubinadamu,tatu nilidhani nyakati mpya,nne nildhanai ilani ya chama itawekwa kando,tano nilidhani hisia za kweli shauri kaishi mjini.....kumbe ilikuwa kama kawaida wabongo tunavyopenda kusikia neno 'ahadi'.
JibuFutaasante kwa kutembelea blogu yangu pia
Karibu mpangala. Nimependa lugha yako.
JibuFuta