UKIMWI una tiba kumbe?


Sikuandika siku kadhaa zilizopita, kipingamizi kikiwa ni uvamizi wa kirusi. Nafurahi kwamba "tabibu" alipatikana, na tiba sahihi ilifanyika, UKIMWI ukasalimu amri.


Shukrani za pekee zimwendee Bwana Minja, msomaji wa blogu (yeye anadai inatosha kuzisoma) na fundi mwanafunzi katika sayansi ya kompyuta. Kwa hakika tunawahitaji sana watu kama hawa katika jamii zetu, watusaidie "kugawana" umasikini wetu.
Minja. Minja kaozea katika teknolojia. Minja. Minja na spana. Minja. Ukienda kwa Minja hutathubutu kuongea siasa. Si tu kwamba hatakusiliza, lakini pia mazingira hayatakuruhusu. Bush kafanyeje, wala hajui na hataki kujua. Ongea teknolojia. Ndugu yangu utakoma. Huo ndio mgawanyo wa kazi unaotutofautisha wenyewe kwa wenyewe.
Ndugu Minja nakushukuru sana.


Nitajaribu kuchukua hatua za dharura, tatizo lisijirudie. Wanasema tubadili tabia ili kuepuka gonjwa lile. Basi huenda tabia yangu ya kunyonya blogu mtandaoni na kuzihamishia kwenye kimeo changu inaniponza.
Muhimu, niweze kuandika.

Maoni

Zilisomwa zaidi wiki hii...

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke-1

Maana ya Saikolojia na Nafasi Yake Katika Jamii -1

Haiba ni nini?

Mambo ya Kuzingatia Unapoandika Wasifu wa Kazi (Curriculum Vitae)

Uislamu ulianza lini?

Tabia za Mtoto wa Miaka 0 – 3 Kimahusiano na Kihisia