Habari za siku ndugu msomaji. Binafsi sijambo. Nafurahi kurejea kibarazani baada ya heka heka za huko na huko. Itoshe kuhusu mimi, nikukaribishe tena humu ndani. Leo ningependa kukusimulia kisa kimoja. Nikuase kwanza, kwamba usilazimike kunielewa vibaya. Sijawa na tabia ya kuona makosa zaidi niwapo mahali ama nikutanapo na watu. Maana siamini kwamba binadamu ana kazi ya kushabikia makosa kuliko jema moja. Nisijitetee sana. Jumapili hii nilipata fursa ya kuhudhuria ibada kwenye kanisa la 'kisomi'. Washirika wa kanisa hili, wengi wao ni wale ambao umande haukuwazuia kuhudhuria shule. Wamesoma. Pamoja na ukweli kwamba wote walikuwa weusi kama mimi, lakini ilikuwa bayana kwamba kiingereza kilikuwa 'nguzo' ya ibada hiyo. Hilo halikuwa tatizo kwangu. Maana inaeleweka kwa wengi wetu kwamba, kusoma kunathibitishwa na umahiri wa kusema kiingereza. Nshazoea hili. Pamoja na ukweli kwamba kiuhalisia kiswahili ndicho kinachotawala madarasani lakini watu hatutaki kuukubali ukweli...
Ni kweli mwaka huu uanakimbia sana na watu tunazidi kuzeeka. Ni furaha kusikia u mzima ni wapi uhuki ulako asali na maziwa....LOL
JibuFutaNashukuru u buheri wa Afya, nami pia afya najivunia.
JibuFutaKila mmoja anaweza kutafsiri mda unavyokwenda kulingana na mazingira aliyopo, nchi ya ahadi lazima siku zikimbie tu! tena siku inapokwisha unakasirika,asali na maziwa yake! wacha we!
Nchi ya kusadikika, daaaa! Siku kama mwezi vile.
muda bwana! ikiwa unasubiri jambo jema unaenda taratibu, ukiwa haujafaniskisha ama haujakamilisha jambo fulani unaenda kwa kasi mno.
JibuFutainaonyesha orodha ya mambo yako bando ndefu ndio maana muda unakuendea haraka.lakini hapana shaka kwa kuwa huko ulikokuwa kuna asali na maziwa basi nadhani mambo siyo mabaya.
karibu tena.
Mwaipopo umenipa tafsiri nzuri ya muda.
JibuFutaKissima, nchi ya kusadikika si halisi. Hii nilimo i halisi na kweli. Inamiminika asali. Mwezi wa asali ulikuwa...
Mwaipopo - inaonekana kama vile ndiyo umemaliza kumsoma Albert Einstein.
JibuFutaBwaya - hiyo nchi inayobubujika maziwa na asali iko wapi tuhamie? Ni ile nchi ya ari mpya, kasi ....na...?
Profesa Masangu, Mwaipopo ni mzee wa nukuzi.
JibuFutaNadhani unaweza kuwa umekosea. Hiyo kasi mpya na ari yake sikujua(ga) kuwa ni kula rasilimali za nchi kwa nguvu mpya.
Nikuja jua, nchi kama nchi ina maziwa tele yanayonywewa na wenyewe hata kama yako kwako mlangoni. Muhimu ni kujinywesha mwenyewe kila unapopata nafasi. Ukisubiri unyweshwe sahau! Wnakimbia na ng'ombe kabisaaa.... Ha ha haaa!