Inasemekana wasomi wanakimbilia siasa. Wanaowaunga mkono wanasema serikali haijali utaalam wao. Inawakejeli kwa malipo kiduchu. Wao, kwa kuona kuwa siasa zinalipa, wanaamua kuzitelekeza fani zao wanakimbilia majimboni kwa lengo la kupata maslahi manono. Inasemwa pia kuwa siasa nayo inawahitaji wataalam kama Maprofesa, Madaktari wa Falsafa na watu kama hao. Kwamba ubobevu wao unatoa mchango mzuri likija suala la maamuzi. Je, ni kweli wanasaidia katika maamuzi? Je, si kweli kwamba kila aina ya ufisadi tunaousikia leo umefanyika mikononi mwa wasomi? Wamesaidia nini? Wanaowapinga, wanasema kuwa elimu yao ilipaswa kujikita katika kuileta jamii maendeleo kupitia fani walizobobea bila kujali serikali inawajali ama la. Kwamba wangejikita vema katika fani zao, ni lazima wangeyapata mafanikio hayo wanayoyafuata katika siasa. Wanasema, kuna ulazima gani wa kila mtu kukimbilia siasa ili kufanikiwa? Je, siasa ndio kila kitu? Je, kukimbilia siasa si dalili ya ufinyu wa elimu yetu? Wanashin...
Ni kweli mwaka huu uanakimbia sana na watu tunazidi kuzeeka. Ni furaha kusikia u mzima ni wapi uhuki ulako asali na maziwa....LOL
JibuFutaNashukuru u buheri wa Afya, nami pia afya najivunia.
JibuFutaKila mmoja anaweza kutafsiri mda unavyokwenda kulingana na mazingira aliyopo, nchi ya ahadi lazima siku zikimbie tu! tena siku inapokwisha unakasirika,asali na maziwa yake! wacha we!
Nchi ya kusadikika, daaaa! Siku kama mwezi vile.
muda bwana! ikiwa unasubiri jambo jema unaenda taratibu, ukiwa haujafaniskisha ama haujakamilisha jambo fulani unaenda kwa kasi mno.
JibuFutainaonyesha orodha ya mambo yako bando ndefu ndio maana muda unakuendea haraka.lakini hapana shaka kwa kuwa huko ulikokuwa kuna asali na maziwa basi nadhani mambo siyo mabaya.
karibu tena.
Mwaipopo umenipa tafsiri nzuri ya muda.
JibuFutaKissima, nchi ya kusadikika si halisi. Hii nilimo i halisi na kweli. Inamiminika asali. Mwezi wa asali ulikuwa...
Mwaipopo - inaonekana kama vile ndiyo umemaliza kumsoma Albert Einstein.
JibuFutaBwaya - hiyo nchi inayobubujika maziwa na asali iko wapi tuhamie? Ni ile nchi ya ari mpya, kasi ....na...?
Profesa Masangu, Mwaipopo ni mzee wa nukuzi.
JibuFutaNadhani unaweza kuwa umekosea. Hiyo kasi mpya na ari yake sikujua(ga) kuwa ni kula rasilimali za nchi kwa nguvu mpya.
Nikuja jua, nchi kama nchi ina maziwa tele yanayonywewa na wenyewe hata kama yako kwako mlangoni. Muhimu ni kujinywesha mwenyewe kila unapopata nafasi. Ukisubiri unyweshwe sahau! Wnakimbia na ng'ombe kabisaaa.... Ha ha haaa!