Yapo mambo mengi katika jamii zetu yaliyofanyika zamani ambayo tukiyatazama twaweza kujifunza mengi. Mengi ya hayo, si sehemu ya jamii za kisasa hivi leo, lakini yalekuwa na msaada wa namna Fulani kwa jamii. Katika jamii ya asili ya wanyaturu, kabila dogo linalopatika katika wilaya ya Singida (na kidogo manyoni), mahusiano kati ya baba na mama yalikuwa na sura tofauti sana na ilivyo leo. Wakati leo hii, wazazi kulala vyumba tofauti huchukuliwa kama ishara ya kufifia kwa mahusiano baina ya wawili hao, kwa Wanyaturu hiyo ilikuwa na maana tofauti. Kikawaida, wazazi wa Kinyaturu hawakupaswa kukaa nyumba moja (sio chumba kimoja, nyumba moja) ndani ya boma. Katika boma analojenga mwanaume kama himaya ya familia yake, alipaswa kuzingatia uwepo wa nyumba mbili ndnai ya boma moja. Baba ambaye ndiye mkuu wa boma, alilala na wanawe wa kiume katika sehemu maalumu ya nyumba inayojulikana kama "Idemu/Ikumbu". Nyumba hiyo ilijitenga pembeni na nyumba kuu alikoishi mama na wanawe wa...
labda! shabaan Robat alituandikia kwamba, usione ukadhani.
JibuFutandio maana siku huzi huwezi kumuuoa mtu mpaka muonajane kwa sababu anaweza kuonekana hendisamu au biutifulu, kumbe kusini mwa jangwa la majani hakuedeki hata kidogo, sasa wewe ukiona sura tu na maumbile unadhani umeona!\
ofcourse, usichokiona chaweza kuwa muhimu saana kuliko unachodhani unakiona. ndio maana huwezi kumuona mungu. eti kizazi cha leo kinamuona kristo wakati alikufa kabla ya video na kamera kuzaliwa, usipende kuamini jua majamaa yanakupiga changa la macho tu! pweeeeee
usipende kumwona papa kavaa nguo nyeupe ukadhani na roho yake ni nyeupe, usiende kuona padri haoi ukadhani hajui utamu wa ngono hasa zile za wizi wizi!!!!
usipende kuona dini zinajifanya kumjua mungu kumbe ndo chanzo cha machafuko duniani.
usipende kuona bwaya anablogu ukadhani ni mwandishi wa habari. usipende kuona kamala naandika hapa ukadhani yu pamoja nawe
usipend kuona kikwete anaendeshwa kwenye magari ya fahara ukadhani karidhika, usipende kuona, usipende kuona, usipende kuona, we ona to, lakini kila ukionacho, usione ukadhani na wala usikose kutazama.
bora kuwa na jicho moja ukaona ya maana kuliko kuwa na mawili ukaanza kuziba moja ili ule chabo kwa .....
thanx, sipende kuona, napenda kutazama
@Bwaya &Kamala: Siutani!:-(
JibuFutaKamala, una kichwa kinachofikiri.
JibuFutaBwaya umenikumbusha sana mwl.wangu wa kemia,alikuwa akipenda kutoa swali ubaoni kisha akasema wale wenye macho ya ndani ndiyo wenye uwezo wa kuuona mtego.Hapa ana maana ni kwa wale wenye kutafakari tu.
JibuFutaNi kweli wengi huamini kwa kile tukuonacho bila ya kutafakari.
Kamala umenena.