Kizazi chetu kinakabiliwa na magonjwa mengi yasiyoonekana. Tunaumwa, na wakati mwingine taabani, lakini hatujui kuwa tunaumwa. Tunatembea, tunakutana na watu, tunapiga picha zenye nyuso zilizochangamka, tunaonekana kufurahia maisha lakini tunateseka na mahangaiko mengi tusiyoweza kuyasema. Tazama kiwango chetu cha ukatili. Haiwezi kuwa kawaida, kwa mfano, kuona mwenzako anaumizwa na wala hujali. Unamuumiza mtu na bado unashangaa kwa nini analalamika. Unamtesa mwenzako kihisia na bado unamdhihaki anapougulia maumivu. Unajiuliza, tumefikaje mahali mwanadamu unaweza kumtesa mwenzako, ukamsababishia maumivu na hujisikii kujutia. Mbaya, wakati mwingine, kiwango hiki cha ukatili kinakuwa kama nyenzo ya kupata tunachokitaka. Tunataka madaraka, tunataka umaarufu, mali na kila kinachotufanya kujione tunnawazidi wengine. Tunakuwa waraibu wa ukatili dhidi ya binadamu wenzetu na hatujisikii kujutia. Tazama kiwango chetu cha ubinafsi. Kwa nini tumepoteza uwezo wa kuafikiria hisia...
labda! shabaan Robat alituandikia kwamba, usione ukadhani.
JibuFutandio maana siku huzi huwezi kumuuoa mtu mpaka muonajane kwa sababu anaweza kuonekana hendisamu au biutifulu, kumbe kusini mwa jangwa la majani hakuedeki hata kidogo, sasa wewe ukiona sura tu na maumbile unadhani umeona!\
ofcourse, usichokiona chaweza kuwa muhimu saana kuliko unachodhani unakiona. ndio maana huwezi kumuona mungu. eti kizazi cha leo kinamuona kristo wakati alikufa kabla ya video na kamera kuzaliwa, usipende kuamini jua majamaa yanakupiga changa la macho tu! pweeeeee
usipende kumwona papa kavaa nguo nyeupe ukadhani na roho yake ni nyeupe, usiende kuona padri haoi ukadhani hajui utamu wa ngono hasa zile za wizi wizi!!!!
usipende kuona dini zinajifanya kumjua mungu kumbe ndo chanzo cha machafuko duniani.
usipende kuona bwaya anablogu ukadhani ni mwandishi wa habari. usipende kuona kamala naandika hapa ukadhani yu pamoja nawe
usipend kuona kikwete anaendeshwa kwenye magari ya fahara ukadhani karidhika, usipende kuona, usipende kuona, usipende kuona, we ona to, lakini kila ukionacho, usione ukadhani na wala usikose kutazama.
bora kuwa na jicho moja ukaona ya maana kuliko kuwa na mawili ukaanza kuziba moja ili ule chabo kwa .....
thanx, sipende kuona, napenda kutazama
@Bwaya &Kamala: Siutani!:-(
JibuFutaKamala, una kichwa kinachofikiri.
JibuFutaBwaya umenikumbusha sana mwl.wangu wa kemia,alikuwa akipenda kutoa swali ubaoni kisha akasema wale wenye macho ya ndani ndiyo wenye uwezo wa kuuona mtego.Hapa ana maana ni kwa wale wenye kutafakari tu.
JibuFutaNi kweli wengi huamini kwa kile tukuonacho bila ya kutafakari.
Kamala umenena.