Nani hushaurika kikweli kweli?

Kila mtu anayo misimamo na imani ambayo kwayo huiishi. Misimamo hii ambayo kimsingi ni falsafa, hujengeka kadiri tukuavyo kulingana na aina ya watu na matukio tunayokumbana nayo.

Falsafa hizi ndizo hutawala namna tunavyoishi na watu, tunavyoyachukulia mawazo yao na hata namna tunavyojichukulia sisi wenyewe.

Inasemekana, katika umri fulani wa makuzi, falsafa hizi huwa hazibadiliki tena. Tunaposhauriwa jambo, kwa mfano, kabla ya kulikubali, hulipambanisha na falsafa zetu. Ikiwa litashahabiana, hulipokea/assimilate na ikiwa litapingana na falsafa zetu, hulipuuza.

Ndio maana kabla hujajitosa kumshauri mtu lolote, chunguza falsafa yake kwanza. Vinginevyo utakuwa unateketeza muda wako bure kumpa 'vidonge vyake' wakati ni wazi hatavielewa hata kama ni kweli unaweza kuwa sahihi kuliko yeye kwa vigezo vyako.

Kimsingi, watu huwa hawashauriki, ila hutafuta kuungwa mkono kile wanachowaza.

Maoni

  1. Kaka ahsante kwa kutueleimisha, nimepita hapa ili nijielewe...

    JibuFuta
  2. kusahaulika naomba urekebishe hiyo

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Zilisomwa zaidi wiki hii...

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke-1

Maana ya Saikolojia na Nafasi Yake Katika Jamii -1

Haiba ni nini?

Uislamu ulianza lini?

Pay $900? I quit blogging