Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2025

Ukiigiza Ukatili, Unakaribisha Tabia ya Ukatili

Picha
Kuna wakati unaweza kufikiri unaigiza msimamo na kejeli kwa maumivu ya mtu, unakuwa na maoni yasiyo na haya kwa mateso ya wenzako ukijua unawafurahisha watu fulani lakini hayo maigizo ya kukosa huruma kwa mwenzako yana uwezekano wa kugeuka tabia kweli na ukawa mtu katili kweli kweli. Michezo, dini na siasa visikuchochee kujiona una haki ya kubeza masaibu wanayopitia wenzako kwa sababu mdogo mdogo mizaha hugeuka ukweli.   Mwaka 1971, Philip Zimbardo, mshunuzi na mwalimu wa Chuo Kikuu cha Stanford, alifanya utafiti maarufu kama  #StanfordPrisonExperiment  akilenga kuchunguza nguvu ya mazingira kwenye tabia.    Utafiti ulivyofanyika   Zimbardo alitengeneza gereza la kuigiza hapo chuoni likiwa na seli, mahali mfungwa angekaa mwenyewe, mahali pa wanyarapa kuishi, mahali wafungwa wangetoka na kuteswa na wanyapara. Washiriki walifanyiwa mchujo wa haiba kuona kama ni watu wenye utimamu wa tabia na hisia.    Kwa njia ya nasibu (random assignment) wanafunzi...

Tabia za Mamlaka kwa Wanyonge Zinavyoweza Kuzalisha Uovu

Picha
Umewahi kujiuliza kwa nini watu huweza kupokea na kutekeleza amri hata zile wanazoamini ni kinyume cha maadili, utu na dhamiri zao? Kwa nini mtu anaweza kuambiwa ‘fanya kitu cha kikatili’ na akatii hata kama amri hiyo inamaanisha mtu kuumia na hata kufa?    Mwanzoni mwa miaka ya 1960, Stanley Milgram wa Chuo Kikuu cha Yale alifanya utafiti maarufu kwa jina la  #TheMilgramExperiment . Milgram alitaka kuangalia nini hasa kinachangia mtu kutii mamlaka hata katika mazingira ambayo utii huo unaweza kusababisha madhara kwa binadamu mwenzake.    Kwa lugha nyingine, nini hasa kilifanya watu kama Hitler waliofahamika wazi ni wakatili wawe na wafuasi waaminifu wanaotekeleza maagizo yao kuumiza watu, kutesa na hata kuwaua?   Utafiti ulivyofanyika   Washiriki wa utafiti huo waliaminishwa wanashiriki utafiti wa kuangalia uhusiajo wa kumbukumbu na ujifunzaji na wao wanashiriki kama ‘walimu.’ Jukumu lao lilikuwa ni kusoma swali na kufanya maamuzi ya kumuadhibu mwanaf...

Malezi yanavyochochea ubabe katika jamii

Picha
Natamani tutafakari jambo hili kwa kina. Nyumbani tumemzoesha mtoto fujo —fimbo, makofi, matusi na aina nyingine za ubabe. Sisi wazazi tunaamini hatuwezi kulinda mamlaka yetu bila kumsababishia mtoto maumivu iwe kwenye mwili wake au hisia zake. Ukiangalia yanayoendelea nyumbani hakuna mazungumzo yenye upendo na mtoto. Tunaamini amani na utulivu kwenye ngazi ya familia ni pale tunapokuwa na watoto wasiofikiri, wasiouliza, wasiothubutu kutofautiana na wazazi ambao ndio mamlaka katika familia.     Shuleni mtoto anakutana na mwalimu anayeamini njia pekee na ya uhakika kulinda heshima na mamlaka yake darasani ni vitisho, fimbo na kila aina ya ubabe kwa mwanafunzi. Ukiangalia mbinu za ufundishaji wake huoni wapi anaamini katika ushirikishwaji wa mwanafunzi. Tangu asubuhi mpaka jioni zoezi linalotawala ni wanafunzi kupokea maelekezo na kuyakariri.    Mwalimu anaamini nidhamu ni pale amani na utulivu vinapotawala darasani. Hii, huenda ndio sababu shule zinahangaika na wapiga...

Kutumia UmahiriHisia (Emotional Intelligence) Kuimarisha Mahusiano

Picha
  Tunamalizia safari yetu ya kujifunza umahirihisia. Tumeangazia maeneo makubwa manne. Kwanza, uelewa wa hisia na sababu zake. Pili, tulitazama namna ya kurekebu hisia zetu . Kisha tukatazama namna tunavyoweza kujenga motisha na hamasa ya kufikia malengo yetu .     Kisha tukaangalia namna umahirihisia unavyotuwezesha kuwasiliana na watu pasipokuzalisha migogoro isiyo na sababu.     Maeneo haya manne ya umahirihisia, yanatafsirika katika mahusiano yetu na watu —namna tunavyowachukulia wasioamini tunachokiamini, namna tunavyowajibu wasiofikiri kile tunachokifikiri, namna tunavyotatua migogoro na maamuzi tunayochukua pale tunapojisikia kuonewa.    Msingi wa mahusiano yenye tija na watu ni uwezo wako wa kujitambua, kutambua namna hisia na tabia zako zinavyoathiri wengine, namna unavyomudu hisia zako lakini pia kiwango chako cha upendo kwa watu. Mtu mwenye #UmahiriHisia hagombani kirahisi. Ukigombana naye anajua namna ya kujinasua na kukuachia ugomvi wako...

Kutumia UmahiriHisia (Emotional Intelligence) Kuelewa na Kuheshimu Hisia za Wenzako

Picha
  Hivi huwa unajiuliza hisia zako zinawaathiri vipi watu wanaokuzunguka? Umewahi kujiuliza ni kwa kiwango gani, mathalani, wivu, husda, fedheha, majuto na hatia vinavyoathiri watu wanaokuzunguka?     Nimewahi kusikia watu wakijisifia kuumiza watu wengine.  “Sijali anajisikiaje shetani yule.” “Kwanza nilikuwa nimekasirika. Usinisumbue.” Haya ni maneno yanayotamkwa na mtu mwenye maumivu makubwa ya kihisia. Huwezi kuwa na umahirihisia ukiwa na maumivu yanayokufanya usijali mwenzako anajisikiaje.   UmahiriHisia unatuwezesha kuwa na uwezo wa kutafakari madhara ya hisia zetu kwa wengine. Kutokujali watu wanaathirika vipi na hisia zako, kujali tu hisia zako na kushindwa kuwaza wengine wanakuonaje, wanakuchukuliaje, uwezekano ni mkubwa kuwa una ulemavu wa hisia —hujali na wala hujisumbui kufikiri madhara ya tabia zako kwa wengine.    Kujifunza kufuatilia mwangwi wa hisia zako kwa wengine ni sehemu muhimu ya darasa la umahirihisia. Mahusiano yako na watu yanahi...

UmahiriHisia (Emotional Intelligence) Unavyochochea Motisha na Kujituma

Picha
Kuna kukosa ari ya kaza. Msimamizi wako asipokufuatilia na kuweka utaratibu wa kukudhibiti ufanye unachopaswa kufanya, hakuna unachoweza kuonesha kama matokeo. Huna msukumo wowote wa kujituma na wala hujisikii hatia.   Hali kama hii inaweza kusabishwa na mengi. Kuna suala la mazingira magumu ya kazi. Hupati vitendea kazi unavyohitaji ili kufanya kazi yako vizuri. Kuna suala la uongozi usiojali hisia zako. Unalalamika na hakuna anayeonekana kusikia. Kuna  mengi yanayoweza kukufikisha mahali ukapoteza motisha ya kazi.    Wengi wanaposikia motisha wanawaza matokeo mazuri unayopata aghalau kutoka kwa mtu kama kichocheo cha kufanya kazi.  “Hapa hatupewi motisha yoyote.”  “Tunafanya kazi na hakuna motisha.” “Toeni motisha muone nitakavyofanya kazi.”   Tunapozungumzia motisha hatuzungumzii kutambuliwa kwa kazi unayofanya, kuonekana, kusifiwa, kupandishwa cheo wala kupewa kitu kama bakhshishi ya bidii yako ya kazi. Motisha ni ile sababu inayoamsha ari ya ...