Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2025

Kutumia UmahiriHisia (Emotional Intelligence) Kuimarisha Mahusiano

Picha
  Tunamalizia safari yetu ya kujifunza umahirihisia. Tumeangazia maeneo makubwa manne. Kwanza, uelewa wa hisia na sababu zake. Pili, tulitazama namna ya kurekebu hisia zetu . Kisha tukatazama namna tunavyoweza kujenga motisha na hamasa ya kufikia malengo yetu .     Kisha tukaangalia namna umahirihisia unavyotuwezesha kuwasiliana na watu pasipokuzalisha migogoro isiyo na sababu.     Maeneo haya manne ya umahirihisia, yanatafsirika katika mahusiano yetu na watu —namna tunavyowachukulia wasioamini tunachokiamini, namna tunavyowajibu wasiofikiri kile tunachokifikiri, namna tunavyotatua migogoro na maamuzi tunayochukua pale tunapojisikia kuonewa.    Msingi wa mahusiano yenye tija na watu ni uwezo wako wa kujitambua, kutambua namna hisia na tabia zako zinavyoathiri wengine, namna unavyomudu hisia zako lakini pia kiwango chako cha upendo kwa watu. Mtu mwenye #UmahiriHisia hagombani kirahisi. Ukigombana naye anajua namna ya kujinasua na kukuachia ugomvi wako...

Kutumia UmahiriHisia (Emotional Intelligence) Kuelewa na Kuheshimu Hisia za Wenzako

Picha
  Hivi huwa unajiuliza hisia zako zinawaathiri vipi watu wanaokuzunguka? Umewahi kujiuliza ni kwa kiwango gani, mathalani, wivu, husda, fedheha, majuto na hatia vinavyoathiri watu wanaokuzunguka?     Nimewahi kusikia watu wakijisifia kuumiza watu wengine.  “Sijali anajisikiaje shetani yule.” “Kwanza nilikuwa nimekasirika. Usinisumbue.” Haya ni maneno yanayotamkwa na mtu mwenye maumivu makubwa ya kihisia. Huwezi kuwa na umahirihisia ukiwa na maumivu yanayokufanya usijali mwenzako anajisikiaje.   UmahiriHisia unatuwezesha kuwa na uwezo wa kutafakari madhara ya hisia zetu kwa wengine. Kutokujali watu wanaathirika vipi na hisia zako, kujali tu hisia zako na kushindwa kuwaza wengine wanakuonaje, wanakuchukuliaje, uwezekano ni mkubwa kuwa una ulemavu wa hisia —hujali na wala hujisumbui kufikiri madhara ya tabia zako kwa wengine.    Kujifunza kufuatilia mwangwi wa hisia zako kwa wengine ni sehemu muhimu ya darasa la umahirihisia. Mahusiano yako na watu yanahi...

UmahiriHisia (Emotional Intelligence) Unavyochochea Motisha na Kujituma

Picha
Kuna kukosa ari ya kaza. Msimamizi wako asipokufuatilia na kuweka utaratibu wa kukudhibiti ufanye unachopaswa kufanya, hakuna unachoweza kuonesha kama matokeo. Huna msukumo wowote wa kujituma na wala hujisikii hatia.   Hali kama hii inaweza kusabishwa na mengi. Kuna suala la mazingira magumu ya kazi. Hupati vitendea kazi unavyohitaji ili kufanya kazi yako vizuri. Kuna suala la uongozi usiojali hisia zako. Unalalamika na hakuna anayeonekana kusikia. Kuna  mengi yanayoweza kukufikisha mahali ukapoteza motisha ya kazi.    Wengi wanaposikia motisha wanawaza matokeo mazuri unayopata aghalau kutoka kwa mtu kama kichocheo cha kufanya kazi.  “Hapa hatupewi motisha yoyote.”  “Tunafanya kazi na hakuna motisha.” “Toeni motisha muone nitakavyofanya kazi.”   Tunapozungumzia motisha hatuzungumzii kutambuliwa kwa kazi unayofanya, kuonekana, kusifiwa, kupandishwa cheo wala kupewa kitu kama bakhshishi ya bidii yako ya kazi. Motisha ni ile sababu inayoamsha ari ya ...

UmahiriHisia (Emotional Intelligence) Unavyosaidia Kurekebu na Kumudu Hisia

Picha
  Tunaendelea na elimu ya hisia. Katika makala yaliyopita , tumejifuza msamiati wa hisia. Mbali na kutofautisha mihemuko na hisia, tumedadisi namna hisia, katika ujumla wake, zinavyobeba ujumbe.     Kila hisia huja na ujumbe fulani. Umahirihisia ukuwezesha kutafakari ujumbe unaobebwa na hisia zako.     Katika makala haya, ningependa tutafakari kwa pamoja namna ya kuzikebu na kuzimudu hisia zetu. Nianze na swali. Unakumbuka mazingira umewahi kujikuta ukifanya maamuzi mabaya kwa sababu hujipa muda wa kupooza hisia zako?  Unakumbuka kusema jambo ukiwa na hasira, kwa mfano, halafu baadae ukajutia? Unamwandikia mpenzi wako maneno makali shauri ya hisia za wivu lakini baadae ukishapoa unagundua hukuwa na sababu ya kusema ulichokisema?   Napenda nukuu moja ya mama anayeitwa Maya Angelou, “Watu wanaweza kusahau ulichokifanya. Watu wanaweza kusahau ulichokisema. Lakini watu hawawezi kusahau ulivyowafanya wakajisikia .” Unaweza kuona uzito wa hisia katika kumbuk...

Kutumia UmahiriHisia (Emotional Intelligence) Kuelewa Unavyojisikia

Picha
Katika utangulizi wetu , nilieleza maana ya umahirihisia na nyanja zake tano. Nilieleza kuwa, ingawa umahirihisia una nyanja hizo tano, ukiyatazama vyema mawanda yake, unaona kuna maeneo makubwa mawili. Eneo la kwanza, ni utambuzi kwa maana ya kuelewa hisia zako, kuzifuatilia na kuzirekebu kwa maana ya kujifunza namna ya kuzimudu zisikuingize kwenye matatizo.     Eneo la pili linategemea eneo la kwanza, kwa maana ya uwezo wa kutumia utambuzi huo wa hisia kuelewa namna ya kuelewa, kutambua na kuheshimu hisia za wengine kwa minajili ya kuboresha mahusiano yako na watu.   Katika sehemu hii ya pili, ninajielekeza kueleza kwa ufupi jinsi gani umahirihisia unaweza kukuzaidia kuzielewa na kuzirekebu hisia zako.     Umewahi kukutana na mtu mwenye uwezo mzuri wa kusoma ujumbe unaobebwa na uso wa mtu? Ukitabasamu, mwingine anaishia kwenye uso huo wenye tabasamu lakini yeye ana uwezo wa kujua kuwa pamoja na tabasamu lako, kuna kitu hakiko sawa.  Unashangaa pamoja na k...

UmahiriHisia (Emotional Intelligence) ni Nini?

Picha
Umewahi kujiuliza kwa nini, wakati mwingine, mtu mwenye akili nzuri, mwenye weledi na uelewa mpana wa mambo, hujikuta na majanga mengi linapokuja suala la namna anavyoishi na watu? Shida ni nini? Iweje mtu aelewe mambo mengine vizuri lakini asindwe mambo madogo kama kuwa msikivu, mvumilivu wa mawazo tofauti, mwenye subira hali inayoweza kumuingiza kwenye magomvi na watu? Wengine tunafikiri tuna misimamo mikali, tumenyoooka na hatujali kutofautiana na nani lakini ukitazama vizuri hiyo inayoitwa misimamo mikali  ni changamoto za kihisia, uwezo mdogo wa kuelewa mitazamo ya wengine, na saa nyingine ni kiburi tu kuwa tunajua kuliko wengine, hawana wanachoweza kutuambia na kadhalika.  Kinyume na tunavyoamini wengi wetu, hisia hubeba maamuzi yetu mengi na ukitazama matatizo yetu mengi ya kitabia unaweza kuona mchango mkubwa wa kushindwa kuzielewa na kuzimudu hisia zetu. Ingawa tunazipuuza, ukweli ni kwamba ukishashindwa kuzishughulikia hisia zako, uwezekano wa kukabiliana na matatizo...