Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2025

Madhara ya Kutoa Ushauri Kienyeji na Kuugeuza Unasihi kuwa Ushauri

Picha
Utamaduni wa (kutoa na kuomba) ushauri umejengeka kwenye misingi ya hekima ya wazee walioona mengi, uzoefu wa mtu mzima unaompa uhalali wa kutoa mwongozo wa kufuata kwa anayemzidi.  Hata tunaposikia unasihi (counselling), aghalabu, mawazo yetu yanaenda kwenye taaluma ya kushauri watu na kuwaambia cha kufanya ili kutatua matatizo yanayowakabili. Wapo, tena wengi, wanaotafsiri ‘counselling’ kama ushauri. Counselling sio ushauri. Katika makala haya, ninajenga hoja kuwa kutoa ushauri ni jambo la hatari na kwamba linaweza kusababisha madhara makubwa kwa anayeshauriwa lakini pia hata anayeshauri.  Kadhalika, ninalenga kuonesha, japo kwa ufupi kuwa hata kwenye unasihi msingi wa kwanza wa kuzingatia kwa mtoa huduma (aliyefuzu) ni kuepuka kabisa kutoa ushauri kwa mtu. Nakusudia kuonesha nini hasa huwa ni malengo ya unasihi. stefanamer/Getty Images Ushauri ni nini?  Unaposema unamshauri mtu unakuwa na maana gani?  Ushauri, kwa kifupi, ni maelekezo mahususi unayompa mtu, maamuz...

Changamoto za kuwanyima watoto kufurahia utoto wao

Picha
  Tunaishi kwenye dunia inayopitia mabadiliko mengi. Mabadiliko haya ya kijamii na kiuchumi, kwa kiasi kikubwa, yamezidisha matarajio tuliyonayo kwa maisha. Ukiacha matarajio mengi tuliyonayo kwetu binafsi, kuna matarajio mengi hata kwa wenzi wetu. Mke, kwa mfano, anatarajia mume awe kila kitu anachokifahamu kuhusu mwanamume. Mume ana kazi ya kuwa mcha Mungu, mtu wa sala, mtafutaji na mchapa kazi hodari, mcheshi, rafiki msikivu, kiongozi bora,     baba mzuri na mume mzuri asiyechelewa kurudi nyumbani. Matarajio haya makubwa yana faida zake lakini pia yana upande wa pili unaochanga migogoro mingi katika familia.   PICHA:  Wikimedia Commons   Hatuishii kuwa na matarajio makubwa kwa wenza wetu. Tunazidisha pia matarajio kwa watoto wetu kiasi cha kuwanyima fursa ya kufurahia utoto wao. Hebu fikiria mtoto asiyeruhusiwa kufanya makosa. Kila analojaribu kufanya, anapodadisi mazingira yake,  anakuwa anatafsirika kama mtoto asiye na nidhamu na adabu kwa wa...

Ukishasahau ulikotoka huwezi kuwa mzazi mzuri

Picha
  Sijui kama umewahi kuwaza kama mimi. Je, mafanikio yetu yanawasaidia watoto kuwa binadamu timamu? Je, uwezo tulionao kiuchumi unawezesha watoto kujifunza tabia zitakazowafanikisha kiuchumi? Kuna namna ninaogopa kuwa huenda tunawanyima watoto wetu fursa ya kujifunza maisha katika uhalisia wake. Nafahamu wapo baadhi ya wazazi wamekulia kwenye familia zinazojiweza kiuchumi. Hata hivyo, hiyo haiondoi ukweli kuwa wengi wetu tumetoka kwenye familia masikini na tumekuwa kizazi cha kwanza kupambana na kuuweza umasikini. Je, tunawaandaa watoto wetu kujikwamua kama tulivyojikwamua sisi?   PICHA: Marlous de Milliano Tunafahamu namna umasikini unavyofedhehesha. Umasikini unafanya maisha yako yasiwe na uchaguzi. Umasikini unakufanya upate kinachopatikana na sio kile unachokihitaji.  Hili, pamoja na ubaya wake, kwa kiasi kikubwa limekuwa kichocheo cha wengi wetu kuwa na hasira kubwa kupambana na umasikini kwa nguvu zote. Bidii ya kazi unayokuwa nayo ni matokeo ya hasira kuwa usi...

Una nguvu ya kupambana na hali iliyokuchosha

Umewahi kujiuliza kwa nini mtu anapigwa, anaumizwa, anadhalilishwa na mpenzi wake na bado haoni kama kuna kitu anaweza kufanya? Mwingine anasitisha uhusiano lakini anapoanzisha mahusiano anakutana na mwingine mwenye tabia zile zile alizozikimbia kwa aliyemwacha. Ili kulitafakari hili, nikusimulie alichokifanya Martin Seligman na Steven Maier mwaka 1965. Washunuzi hawa waliwatia mbwa kifungoni kwa kuwafungia kwenye kizimba kisichowaruhusu kutoka. Mle ndani kizimbani mbwa walipigwa shoti ya umeme mfululizo iliwapa maumivu makali. Hata pale ambapo mbwa angefanya majaribio ya kutoroka asingeweza. Kizimba kilikuwa imara. Kilichowashangaza Seligman na Maier ni kwamba hata pale walipofungua mlango wa kizimba kuwaruhusu watoke, ingawa mbwa wale walilia kwa uchungu, wakilalamika na kutia huruma, hawakuthubu kujaribu kutoka pamoja na maumivu makali ndani ya kizimba. Hali ilikuwa tofauti kwa kundi jingine la mbwa lililokuwa limefungiwa kwenye kizimba kisicho na shoti ya umeme au kilichokuwa na uw...