Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2025

Jifunze Uhusiano wa Malezi na Vilema vya Haiba (Personality Disorders)

Picha
Kizazi chetu kinakabiliwa na magonjwa mengi yasiyoonekana. Tunaumwa, na wakati mwingine taabani, lakini hatujui kuwa tunaumwa. Tunatembea, tunakutana na watu, tunapiga picha zenye nyuso zilizochangamka, tunaonekana kufurahia maisha lakini tunateseka na mahangaiko mengi tusiyoweza kuyasema.   Tazama kiwango chetu cha ukatili. Haiwezi kuwa kawaida, kwa mfano, kuona mwenzako anaumizwa na wala hujali. Unamuumiza mtu na bado unashangaa kwa nini analalamika. Unamtesa mwenzako kihisia na bado unamdhihaki anapougulia maumivu. Unajiuliza, tumefikaje mahali mwanadamu unaweza kumtesa mwenzako, ukamsababishia maumivu na hujisikii kujutia.    Mbaya, wakati mwingine, kiwango hiki cha ukatili kinakuwa kama nyenzo ya kupata tunachokitaka. Tunataka madaraka, tunataka umaarufu, mali na kila kinachotufanya kujione tunnawazidi wengine. Tunakuwa waraibu wa ukatili dhidi ya binadamu wenzetu na hatujisikii kujutia. Tazama kiwango chetu cha ubinafsi. Kwa nini tumepoteza uwezo wa kuafikiria hisia...

Unayafahamu Anayopitia Mwanao na Hakuambii?

Picha
Kama sehemu ya wajibu wangu wa kitaaluma, huwa ninaandaa, kuendesha na kutathmini mafunzo ya ulinzi wa mtoto kwa walimu, wanafunzi na wazazi kwenye shule mbalimbali nchini. Nimeendesha mafunzo hayo kwa shule nyingi hususani za binafsi na zile zinazoendeshwa na mashirika binafsi na kidini.     Hivi karibuni nilipata bahati hiyo kwenye shule moja kubwa inayoendeshwa na shirika moja la kitawa. Imani tuliyonayo wazazi wengi kwa shule hizi ni mfumo madhubuti wa malezi unaowahakikishia watoto usalama wao. Ingawa ni kweli matarajio ya wazazi wengi ni ufaulu mzuri, hili la malezi yenye kumjenga mtoto kimaadili ni kubwa zaidi.   Siku hiyo, Ijumaa, kabla ya kuzungumza na wazazi Jumamosi yake, nilipata wasaa wa kusema na watoto wa kidato cha kwanza na cha pili. Madhumuni ya kuanza na watoto ni kupata uzoefu halisi ninaoweza kuutumia kama rejea kwenye mazungumzo na wazazi. Nafahamu sisi wazazi huwa hatupokei jambo kirahisi hasa linapoonekana halina uhalisia. Ninapokuwa na mifano hali...

ChatGPT Inapoaminika Kuliko Mzazi

Picha
Jioni moja wiki iliyopita nilikuwa Instabul. Huu ni mgahawa mmoja maarufu jijini Dar es salaam. Hapa nafanya nazungumza na Damari, mwanafunzi wa shahada katika taasisi moja ya elimu ya juu jijini Dar es salaam. Sikumwuuliza umri lakini nakadiria ana miaka 21. Kikao chetu kimezaliwa na kipindi nilichokuwa nimekifanya asubuhi hiyo kwenye kituo kimoja cha televisheni.   Tulizungumza kwa kirefu suala alilokuwa nalo na tufikia muafaka. Kisha nilimwuuliza swali ambalo huwa nawauliza ‘wadogo’ zake ninapokuwa naendesha mafunzo ya malezi shuleni.  "Nani ni rafiki yako wa karibu?" Nalenga kujua anamwamini nani.  Hakufikiri mara mbili akanijibu, "ChatGPT!” Sikuzuia mshangao. Jambo hili, kwa hakika, lilinisumbua. Sikuwahi kufikiri ChatGPT ingewahi kuwa rafiki wa mtu. Kama huifahamu, ChatGPT ni programu tumizi inayotumia teknolojia ya akili mnemba. Imentegenezwa kuwezesha mazungumzo yanayolingana na unachoulizia.    “Umesema ChatGPT ndio rafiki yako?” “Ndio. Rafiki ninayemwa...

Ukifikiri Upendo ni Vitu Utamkinai Anayekupenda

Picha
Juzi naongea na kijana mmoja, umri nakadiria kavuka miaka thelathini, ananiambia ameanza kuhisi kama vile hakuumbiwa mapenzi. Ukisikia mtu anatoa kauli nzito hivi ujue kuna jambo. Kudodosa, kumbe, kayapambania mapenzi na yamekaribia kumtoa roho. Kila anayempenda kwa dhati anaishia kumwacha hewani.     Haelewi afanye nini.   “Hawa wanawake wanataka nini?” Kaniuliza. Tuliongea mengi. Naomba nikushirikishe, japo kwa muhtasari, maudhui ya mazungumzo yetu.    Picha: Tony Cordoza   |  Getty Images Tumeanza kuwa na kizazi cha vijana werevu, watafutaji, wenye uwezo mkubwa wa kutafuta pesa lakini wenye hisia kificho, wasiojali hisia na wasio na haja ya kina cha mahusiano.  Hiki ni kizazi, aghalabu, kilichozaliwa na kizazi cha wazazi wasomi, wenye maarifa zaidi na pesa zaidi kuliko kizazi kilichopita. Tunatumia muda mwingi kazini, kwenye biashara, na shughuli nyingine za kutafuta vitu. Ukiangalia kwa haraka unaona hiki ni kizazi chenye watu wenye kazi ...

Ulionao ni watoto au mitoto?

Picha
  “Wenzangu nyie mnafanyaje watoto wawasikilize?” analalamika mama Rehema. “Hata sijui nilimkosea nini Mungu! Hii niliyonayo ni mitoto.” Namuuliza kwa nini? Kama mtu asiyeamini anaulizwa swali la kijinga ananijibu: “Haina akli, mijinga, mitundu, mikorofi, pasua kichwa kazi kunitia hasara tu,” anasema kwa hasira.    Kanisimuliza juzi kwenye mtihani wa nusu muhula mwanae mkubwa kawa wa thelathini na nane kati ya watoto arobaini darasani mtihani. “Huwezi amini hata sijashangaa. Mtoto wa Asha kapata A anawaongozea darasani!”    Kwa muda mfupi niliokaa pale kwake, watoto ni kama watumwa ni mwendo wa kelele na amri  kwenda mbele.  “Mama Rehema si ungerekodi tu amri ziwe zinatokea kwenye spika?” namwambia kwa kejeli baada ya kuona anatumia nguvu kubwa kutoa amri zile zile.  “Rehema! Unafanya nini?”  “Samweli? Hujanisikia?”  “We Rehema uko wapi hebu njoo nipe rimoti”   Mama Rehema anawakilisha tabia zetu wazazi wengi. Ingawa tunawaita ...