Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2025

Ukifikiri Upendo ni Vitu Utamkinai Anayekupenda

Picha
Juzi naongea na kijana mmoja, umri nakadiria kavuka miaka thelathini, ananiambia ameanza kuhisi kama vile hakuumbiwa mapenzi. Ukisikia mtu anatoa kauli nzito hivi ujue kuna jambo. Kudodosa, kumbe, kayapambania mapenzi na yamekaribia kumtoa roho. Kila anayempenda kwa dhati anaishia kumwacha hewani.     Haelewi afanye nini.   “Hawa wanawake wanataka nini?” Kaniuliza. Tuliongea mengi. Naomba nikushirikishe, japo kwa muhtasari, maudhui ya mazungumzo yetu.    Picha: Tony Cordoza   |  Getty Images Tumeanza kuwa na kizazi cha vijana werevu, watafutaji, wenye uwezo mkubwa wa kutafuta pesa lakini wenye hisia kificho, wasiojali hisia na wasio na haja ya kina cha mahusiano.  Hiki ni kizazi, aghalabu, kilichozaliwa na kizazi cha wazazi wasomi, wenye maarifa zaidi na pesa zaidi kuliko kizazi kilichopita. Tunatumia muda mwingi kazini, kwenye biashara, na shughuli nyingine za kutafuta vitu. Ukiangalia kwa haraka unaona hiki ni kizazi chenye watu wenye kazi ...

Hulka ya Mwanadamu Kujikweza na Kukwepa Wajibu

Picha
Umewahi kujiuliza kwa nini mtu akifanikiwa jambo (biashara, kazi, elimu, siasa nk) anataka aonekane ana bidii, ana uwezo na kitu cha tofauti kinachomtofautisha na wengine? Kwa nini, kwa mfano, ikitokea kinyume, mtu akashindwa, akafanya vibaya, hutaka ionekane kuna watu wanamkwamisha, kuna upinzani, kuna wabaya wake na inakuwa nadra kukubali huenda tabia zake mwenyewe zinamgharimu? Mwaka 1978, washunuzi Berglas na Jones waliwatumia wanafunzi wa chuo kuichunguza dhana hii. Makundi mawili ya wanafunzi yalipewa 'puzzle'— fumbo linalohitaji akili kulifumbua. Kundi A walipewa fumbo rahisi. Halikuhitaji kufikiri sana. Kundi B wakapewa fumbo gumu (lisilowezekana hata ukeshe nalo). Makundi yote yalipewa maelekezo kuwa wakihitaji kuboresha uelewa ili wafumbue fumbo wanaweza kuomba kidonge kinachoitwa Actavil lakini wakiona wanahitaji kidonge cha Pandocrin kinachopunguza uelewa pia wangeweza kuomba. Wakati zoezi kiliendelea, 80% ya washiriki wa kundi A (wenye fumbo rahisi) waliomba kido...