Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2025

Ukifikiri Upendo ni Vitu Utamkinai Anayekupenda

Picha
Juzi naongea na kijana mmoja, umri nakadiria kavuka miaka thelathini, ananiambia ameanza kuhisi kama vile hakuumbiwa mapenzi. Ukisikia mtu anatoa kauli nzito hivi ujue kuna jambo. Kudodosa, kumbe, kayapambania mapenzi na yamekaribia kumtoa roho. Kila anayempenda kwa dhati anaishia kumwacha hewani.     Haelewi afanye nini.   “Hawa wanawake wanataka nini?” Kaniuliza. Tuliongea mengi. Naomba nikushirikishe, japo kwa muhtasari, maudhui ya mazungumzo yetu.    Picha: Tony Cordoza   |  Getty Images Tumeanza kuwa na kizazi cha vijana werevu, watafutaji, wenye uwezo mkubwa wa kutafuta pesa lakini wenye hisia kificho, wasiojali hisia na wasio na haja ya kina cha mahusiano.  Hiki ni kizazi, aghalabu, kilichozaliwa na kizazi cha wazazi wasomi, wenye maarifa zaidi na pesa zaidi kuliko kizazi kilichopita. Tunatumia muda mwingi kazini, kwenye biashara, na shughuli nyingine za kutafuta vitu. Ukiangalia kwa haraka unaona hiki ni kizazi chenye watu wenye kazi ...

Ulionao ni watoto au mitoto?

Picha
  “Wenzangu nyie mnafanyaje watoto wawasikilize?” analalamika mama Rehema. “Hata sijui nilimkosea nini Mungu! Hii niliyonayo ni mitoto.” Namuuliza kwa nini? Kama mtu asiyeamini anaulizwa swali la kijinga ananijibu: “Haina akli, mijinga, mitundu, mikorofi, pasua kichwa kazi kunitia hasara tu,” anasema kwa hasira.    Kanisimuliza juzi kwenye mtihani wa nusu muhula mwanae mkubwa kawa wa thelathini na nane kati ya watoto arobaini darasani mtihani. “Huwezi amini hata sijashangaa. Mtoto wa Asha kapata A anawaongozea darasani!”    Kwa muda mfupi niliokaa pale kwake, watoto ni kama watumwa ni mwendo wa kelele na amri  kwenda mbele.  “Mama Rehema si ungerekodi tu amri ziwe zinatokea kwenye spika?” namwambia kwa kejeli baada ya kuona anatumia nguvu kubwa kutoa amri zile zile.  “Rehema! Unafanya nini?”  “Samweli? Hujanisikia?”  “We Rehema uko wapi hebu njoo nipe rimoti”   Mama Rehema anawakilisha tabia zetu wazazi wengi. Ingawa tunawaita ...

Hulka ya Mwanadamu Kujikweza na Kukwepa Wajibu

Picha
Umewahi kujiuliza kwa nini mtu akifanikiwa jambo (biashara, kazi, elimu, siasa nk) anataka aonekane ana bidii, ana uwezo na kitu cha tofauti kinachomtofautisha na wengine? Kwa nini, kwa mfano, ikitokea kinyume, mtu akashindwa, akafanya vibaya, hutaka ionekane kuna watu wanamkwamisha, kuna upinzani, kuna wabaya wake na inakuwa nadra kukubali huenda tabia zake mwenyewe zinamgharimu? Mwaka 1978, washunuzi Berglas na Jones waliwatumia wanafunzi wa chuo kuichunguza dhana hii. Makundi mawili ya wanafunzi yalipewa 'puzzle'— fumbo linalohitaji akili kulifumbua. Kundi A walipewa fumbo rahisi. Halikuhitaji kufikiri sana. Kundi B wakapewa fumbo gumu (lisilowezekana hata ukeshe nalo). Makundi yote yalipewa maelekezo kuwa wakihitaji kuboresha uelewa ili wafumbue fumbo wanaweza kuomba kidonge kinachoitwa Actavil lakini wakiona wanahitaji kidonge cha Pandocrin kinachopunguza uelewa pia wangeweza kuomba. Wakati zoezi kiliendelea, 80% ya washiriki wa kundi A (wenye fumbo rahisi) waliomba kido...

Unalea watoto au unafuga watoto?

Picha
Kila siku saa 12 jioni, Mah’mood mwenye miaka 12 hutoka shule anakosoma moja kwa moja kwenda nyumbani. Mah’mood  anawajua wazazi. Hawawezi kuthubutu kumruhusu kuchelewa nyumbani hata dakika tano. Jaribio lolote la kuchelewa litakaribisha matusi, ukali, na ikibidi kiboko bila maelezo yoyote.  Mah’mood anatamani kuwa mchezaji hodari wa mpira. Ndoto hii imekatishwa baba yake alimwambia, “Hutakula mpira, soma uwe mwanasheria. Hutaki acha shule. Kila Mah’mood anapouliza swali, jibu huwa ni kama limerekodiwa mahali, “nyamaza, wewe ni mtoto.” Kadiri miaka inavyoenda, Mah’mood alizidi kuwa mnyonge na kujiamini kwake. Ukiongea na Mah’mood unaweza kuhisi ni jasiri. Lakini ukisikiliza vizuri unagundua ana unyonge unaoua utu wake, ndoto zake, na uhuru wa kuwa yeye. Je, haya ni malezi au ufugaji? Je, Mah’mood analelewa au anaishi na wazazi wake kama mfugo? Jamii zetu zinaamini mno katika utii na nidhamu. Tunafikiri bila nidhamu iliyopindukia, utii usiohoji basi mtoto hawezi kufanikiwa...