Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2015

Tabora wamemsamehe Lowassa, au ni dalili za kukubalika kwa UKAWA?

Picha
Matokeo ya utafiti mdogo uliofanywa na mwandishi wa makala haya katika mitaa ya mji wa Tabora jioni ya leo, umeonesha kwamba kuna ushindani mkali kati ya Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Ufisadi wa Richmond, Edward Lowassa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk Wilbroad Slaa, kama uchaguzi mkuu ungefanyika kati ya saa 10 – 12:30 jioni hii. Matokeo hayo yanaonesha kwamba Lowassa ana asilimia 28 na Dk Wilbroad Slaa angepata asilimia 22.